Social Icons

Wednesday, May 30, 2012

new hit: ze drinkie ft king charles-cheka kidogo

the song was produced at Rocfame music,by Hans Q, the song is a collaboration of Tanzanian upcoming rapper with RNB legend King Charles. its now aired out on different stations examples, clouds TV, EATV and various radios and Tv stations.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

TABIA HII MPAKA LINI??????

MTOTO wa siku moja mnamo Mei 24, mwaka huu ameokotwa katika makaburi ya Vingunguti, Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam akiwa ndani ya mfuko wa rambo.

Taarifa zilizopatikana katika eneo la tukio zilidai kuwa, mtoto huyo alisikika akilia na wasamaria ambao siku hiyo usiku walienda na kumkuta akiwa katika mfuko mweusi huku mbwa wakimnyemelea.

Mtoto huyo wa kike baada ya kuokolewa na wasamaria wema alipelekwa kwenye kituo cha afya kiitwacho Afya Bora ambapo wafanyakazi wake, Catherine Shayo na Magreth Masanja walimpa huduma ya kwanza kisha wakatoa taarifa Kituo cha Polisi Buguruni na kupewa kumbukumbu namba BUG /RB/6238/2012.

Baadaye mtoto huyo mchanga alipelekwa katika Hospitali ya Amana na PC Nel.

Uchunguzi unaonesha kwamba, maeneo ya Buguruni na Vingunguti yanaongoza kwa utupaji watoto ambapo Aprili 27 na Mei 4, mwaka huu watoto wawili waliokotwa mmoja akiwa amefariki.
Na Makongoro Oging'
Global Publisher
Note: Jamani wadada mpaka lini tabia hii, mbona tunakua wanyama hivi? yani inasikitisha kwa kweli.
Kwa nini mnafanya ngono zembe halafu hamtaki kukubali matokeo? Walaaniwe wote wanaotoa mimba au kutupa vichanga kama hivi,karne hii si ya kupata mimba za bahati mbaya, kuna njia za kila aina za uzazi wa mpango ili kuzuia mimba zisizotarajiwa zinazoleta maafa kama haya. Kuna watu wanalia usiku na mchana kuomba Mungu wapate watoto wakati wengine mwawatupa.
Ole wenu wenye tabia hizo damu za hawa watoto zitawaandama siku zote za maisha yenu.
Nimeumia sana.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

WEMA SEPETU AVISHWA PETE YA UCHUMBA NA MWANAMUZIKI WA MACHOZI BAND.....

                                                    Mwinyi wa Machozi Band amvisha pete ya uchumba Wema Sepetu.
Tukio hilo limetokea jana usiku katika ukumbi wa Maisha Club.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Usafi wa nywele zako

 IKIWA utaosha nywele zako kama kawaida na baadaye kutumia chanuo ama brash katika kuzibana, wakati mwingine unaweza kusababisha kukatika au hata kuathiri ukuaji wa nywele zako.

 Hata hivyo, kwa kufuata ushauri unaweza kuepukana na tatizo hilo na hivyo kusababisha nywele zako kujaa na kukua vyema.  Fuata hizi dondoo rahisi ambazo ili kuhakikisha unasaidia sio kuua nywele zako bali kuzikuza na kuzifanya zinawiri. Ikiwa unatumia mafuta ya jeli, umakini unahitajika katika kuziosha nywele zako. Kama unatumia jeli ya nywele katika mtindo wako, hakikisha unaosha vizuri na kuondoa jeli yote kabla ya  kulala. Unapolala na jeli au urembo mwingine unaofanana nayo, unasababisha kuziba kwa tundu za nywele katika ngozi ya kichwa.

 Kitendo hicho mbali na kuzuia kupumua kwa ngozi ya kichwa pia huchangia kuzuia nywele chipukizi kuota katika ngozi ya kichwa. Kuwa makini na shampoo za madukani Mara nyingi baadhi ya watengenezaji wa vipodozi huweka maslahi mbele bila kuangalia athari zinazoweza kuwapata watumiaji wa bidhaa zao. Kwani kuna baadhi ya shampoo huwa na kemikali hatari kwa ngozi. Hivyo ni vyema zaidi ikiwa utakuwa na uelewa wa kutosha kuhusiana na aina hiyo ya kipodozi. Pendelea zaidi kutumia herbal shampoo.

 Si hivyo tu wakati mwingine vipodozi vya bei rahisi huwa na kasoro, hivyo ni vyema kupata ushauri kutoka kwa wataalamu wa nywele kujua ni aina gani ya shampoo ni sahihi kwa nywele zako. Kinyume cha hapo unaweza kuishia kuathiri nywele na ngozi yako bila ya mwenyewe kufahamu. Epuka kubana nywele mara kwa mara Ubanaji wa nywele hasa kuelekea mgongoni mara nyingi huhatarisha maisha ya nywele zako hasa za usoni. Kwani kiteno cha kuzibana husababisha kuvutwa kwa nywele na hivyo kusabisha kukatika hasa kwa zile zilizo hafifu.

 Usichane nywele zikiwa mbichi Zinapokuwa mbichi nywele huwa na uwezekano mkubwa wa kukatika hasa pale zinapochanwa au kufutwa kwa taulo gumu. Ni vyema ukaacha zikauke kwa upepo na baada ya hapo unaweza kuzichana. Katika hili kama utakuwa unatumia ‘conditioner’hakikisha husugui katika nywele na badala yake tumia kwa kupaka. Ikiwa kama nywele zako zimekatika na hazilingani, ni vyema ukakata ncha ili kuzisawazisha. Hii husaidia kuzifanya zikue vizuri na pia kuondoa uwezekano wa kukatika mara zinapoingia maji.

Hasa kwa zile zenye ‘relaxer’.   Chochea ukuaji wa nywele zako kwa kuzichana Unapochana nywele zako hakikisha unatumia shanuo la mbao au kitana chenye meno yaliyoachana. Hakikisha nywele zako zinakuwa kavu. Usizivute sana kwani pamoja kusababisha maumivu pia huleta uwezekano wa kukatika.

 Jambo la muhimu katika uchanaji wa nywele, husaidia kuchochea mzunguko wa damu katika ngozi ya kichwa na pia husaidia kukua kwa nywele. Imarisha umaridadi wa nywele zako IKIWA utaosha nywele zako kama kawaida na baadaye kutumia chanuo ama brash katika kuzibana, wakati mwingine unaweza kusababisha kukatika au hata kuathiri ukuaji wa nywele zako

. Hata hivyo, kwa kufuata ushauri unaweza kuepukana na tatizo hilo na hivyo kusababisha nywele zako kujaa na kukua vyema.  Fuata hizi dondoo rahisi ambazo ili kuhakikisha unasaidia sio kuua nywele zako bali kuzikuza na kuzifanya zinawiri. Ikiwa unatumia mafuta ya jeli, umakini unahitajika katika kuziosha nywele zako. Kama unatumia jeli ya nywele katika mtindo wako, hakikisha unaosha vizuri na kuondoa jeli yote kabla ya  kulala. Unapolala na jeli au urembo mwingine unaofanana nayo, unasababisha kuziba kwa tundu za nywele katika ngozi ya kichwa.

 Kitendo hicho mbali na kuzuia kupumua kwa ngozi ya kichwa pia huchangia kuzuia nywele chipukizi kuota katika ngozi ya kichwa. Kuwa makini na shampoo za madukani Mara nyingi baadhi ya watengenezaji wa vipodozi huweka maslahi mbele bila kuangalia athari zinazoweza kuwapata watumiaji wa bidhaa zao. Kwani kuna baadhi ya shampoo huwa na kemikali hatari kwa ngozi. Hivyo ni vyema zaidi ikiwa utakuwa na uelewa wa kutosha kuhusiana na aina hiyo ya kipodozi. Pendelea zaidi kutumia herbal shampoo. Si hivyo tu wakati mwingine vipodozi vya bei rahisi huwa na kasoro, hivyo ni vyema kupata ushauri kutoka kwa wataalamu wa nywele kujua ni aina gani ya shampoo ni sahihi kwa nywele zako. Kinyume cha hapo unaweza kuishia kuathiri nywele na ngozi yako bila ya mwenyewe kufahamu. Epuka kubana nywele mara kwa mara Ubanaji wa nywele hasa kuelekea mgongoni mara nyingi huhatarisha maisha ya nywele zako hasa za usoni.

 Kwani kiteno cha kuzibana husababisha kuvutwa kwa nywele na hivyo kusabisha kukatika hasa kwa zile zilizo hafifu. Usichane nywele zikiwa mbichi Zinapokuwa mbichi nywele huwa na uwezekano mkubwa wa kukatika hasa pale zinapochanwa au kufutwa kwa taulo gumu. Ni vyema ukaacha zikauke kwa upepo na baada ya hapo unaweza kuzichana. Katika hili kama utakuwa unatumia ‘conditioner’hakikisha husugui katika nywele na badala yake tumia kwa kupaka. Ikiwa kama nywele zako zimekatika na hazilingani, ni vyema ukakata ncha ili kuzisawazisha. Hii husaidia kuzifanya zikue vizuri na pia kuondoa uwezekano wa kukatika mara zinapoingia maji. Hasa kwa zile zenye ‘relaxer’.   Chochea ukuaji wa nywele zako kwa kuzichana Unapochana nywele zako hakikisha unatumia shanuo la mbao au kitana chenye meno yaliyoachana.

 Hakikisha nywele zako zinakuwa kavu. Usizivute sana kwani pamoja kusababisha maumivu pia huleta uwezekano wa kukatika.  Jambo la muhimu katika uchanaji wa nywele, husaidia kuchochea mzunguko wa damu katika ngozi ya kichwa na pia husaidia kukua kwa nywele
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

MUACHENI MUNGU AITWE MUNGU

HEBU mwacheni Mungu aitwe Mungu! Hatimaye habari njema kutoka katika Hospitali ya Saifee iliyopo jijini Mumbai, India anakotibiwa staa wa filamu za Kibongo, Sadick Juma Kilowoko ‘Sajuki’ zinatia faraja kwa Watanzania.

ANYANYUKA KITANDANI, AONGEA
Habari hizo njema zinaeleza kuwa Sajuki aliyeambatana na mkewe, Wastara Juma na kaka yake, hatimaye ameweza kunyanyuka kitandani na kuongea tofauti na siku aliyoondoka Bongo na mwanzoni alipofikishwa hospitalini hapo.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda, mwishoni mwa wiki iliyopita kwa njia ya simu, Wastara alisema Sajuki alikuwa amepata nafuu na hali siyo mbaya kwani alikuwa na uwezo wa kuzungumza hivyo akampa simu ili azungumzie afya yake yeye mwenyewe jinsi anavyojisikia.
SAJUKI LAIVU
Sajuki alipopewa simu alianza kwa kuwashukuru wale wote wanaomuombea dua na kujitolea kwa hali na mali ili kuokoa uhai wake.
“Namshukuru sana Mungu naendelea vizuri. Nilichukuliwa vipimo na nikabainika kuwa na uvimbe mwingi sehemu mbalimbali tumboni.
“Madaktari walibaini kuwepo kwa uchafu kwenye mapafu. Mwanzoni waligundua nina tatizo la kupumua na kukaukiwa damu.
“Wamelishughulikia hilo kwanza na hapa nilipo nimezungukwa na madawa, kwa kweli najisikia nafuu,” alisema Sajuki kwa sauti ya kukwaruza.
MADAKTARI
Sajuki alisema alipokelewa vizuri lakini kabla ya kuanza matibabu ya uvimbe tumboni, madaktari walilazimika kumtibu kwanza tatizo la damu na pumzi hivyo matibabu ya kilichompeleka hospitalini hapo (uvimbe) yakawekwa pembeni.
WASTARA ATIA NENO
Kwa upande wake, Wastara alisema kuwa Sajuki alipaswa kupatiwa matibabu kwa wiki mbili ndipo warejee nyumbani lakini kwa hali halisi inaonekana watakaa zaidi kwani tayari wiki mbili zimekatika.
MATIBABU YAANZA
Wastara alisema kuwa baada ya kumalizika kwa tatizo la pumzi na kupungukiwa damu, madaktari wameanza vipimo vya tatizo la uvimbe na kusisitiza kuwa uzi ni uleule wa kumwombea mumewe ili arejee katika siha njema.
TUMEFIKAJE HAPA?
Sajuki alianza kusumbuliwa na uvimbe mwaka jana ulioanzia mkononi na baadaye ndani ya mwili kwenye ini na sasa madaktari wanasema siyo kwenye ini tu bali na sehemu nyingine tofauti za tumboni.
Kama alivyosema Wastara, tuzidi kumuombea dua Sajuki ili arejee katika ulingo wa filamu aendelee kutuelimisha na kutuburudisha tunapokuwa majumbani mwetu.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

UMEAMUA KUINGIA KWENYE MAPENZI SASA?

UAMUZI wa kuingia kwenye uhusiano wa kimapenzi si sawa na kufanya uchaguzi wa aina ya chakula unachopenda kula. Haufanani na uamuzi wa kuchagua muda wa kulala. Haufanani na kitu chochote kile.
Ni uamuzi makini, ambao unahitaji utulivu na uamuzi wa ndani. Si kukurupuka, maana mwisho wake unaweza kuwa machozi. Hebu jiulize, wewe ambaye unataka kuanzisha uhusiano wa kimapenzi upo tayari?
Suala la utayari halikuhusu wewe kama wewe kwa uamuzi binafsi na hisia zako za ndani pekee, lazima uwe na sifa muhimu ambazo zinakidhi wewe kuwa na mwenzi. Tupo pamoja marafiki?
Yapo mambo ya msingi ambayo lazima yawe yametimia kwako, ndipo uwe na hadhi ya kuwa mpenzi wa mtu. Wanasaikolojia ya Uhusiano, wameelekeza wazi vipengele muhimu ambavyo kijana anapaswa kuvizingatia kabla hajaamua kuingia katika uhusiano wa kimapenzi.
Hata hivyo, tafiti mbalimbali zinaonesha kuwa vijana wengi wanaobalehe au kuelekea kubalehe huwa hawafahamu vipengele hivyo muhimu na hata hao wachache waliopata elimu hiyo elekezi bado hujikuta wakishindwa kufuata taratibu hizo kulingana na mazingira.
Vipo vitu vingi vya kuzingatia, lakini nitafafanua vile vya msingi zaidi, ambavyo vitakuongoza wewe kijana kabla ya kuamua kuingia kwenye uhusiano.
Ni mada nzuri zaidi kwa vijana ambao bado hawajaanza uhusiano, lakini hata kwa aliyeanza, itamsaidia kujua yupo katika kundi gani na nini cha kufanya. Lazima kuna kitu cha kujifunza katika mada hii. Twende darasani.

SUALA LA UMRI
Hili ni la kwanza kati ya yale muhimu zaidi ya kuzingatiwa, lazima uangalie una umri gani? Inawezekana ukawa na umri ambao unadhani una uwezo mkubwa wa kupanga na kuamua mambo yako lakini kumbe siyo!
Unaweza ukaingia katika uhusiano, ukadumu humo kwa muda mrefu sana, lakini wakati huo ukiendelea kukua kiakili, hapo sasa ndipo utakapogundua kuwa kuna makosa uliyofanya awali.
Inashauriwa kwamba vijana ambao wana umri chini ya miaka 18, wasijiingize kabisa katika uhusiano. Huu ni ushauri na mahali pengine siyo ushauri ni lazima! Kama unajijua upo chini ya umri huu, achana kabisa na mapenzi, huu ni muda wako wa kupanga maisha yako ya baadaye.

KWA WANAFUNZI...
Inawezekana ukawa na umri zaidi ya miaka 18, lakini ukawa masomoni, je unaruhusiwa kuwa na mpenzi? Jibu ni hapana...wewe uliye masomoni hususan Elimu ya Msingi na Sekondari hushauriwi kuwa katika uhusiano kwa kipindi hiki. Masomo ni magumu sana kwa ‘levo’ hii na inawezekana ukashindwa kufanya mitihani yako vizuri kutokana na kuwaza mambo mawili kwa wakati mmoja.
Kimsingi ni vitu viwili tofauti ambavyo havichanganyiki. Hii siyo amri, ni ushauri tu! Kama kweli unataka kufanikiwa katika maisha yako ya baadaye, soma kwanza achana na mambo ya mapenzi katika kipindi hiki.
Andaa maisha yako kwanza. Siku moja ukiwa mitaani baada ya kumaliza masomo, ikiwa utabahatika kusoma makala haya kwa mara nyingine gazetini, mtandaoni au hata kwenye kitabu, utajuta na inawezekana ukalia, wakati huo muda utakuwa umeshapita!

FEDHA INAHUSIKA?
Mapenzi na fedha ni vitu viwili tofauti rafiki zangu, lakini kuna wakati fedha inakuwa na nafasi yake katika mapenzi. Siyo kwa maana ya kuhonga au kununua penzi, lakini kwa ajili ya mahitaji ya hapa na pale.
Sasa jiulize, ikiwa wewe ni mwanafunzi, unayetegemea kupewa fedha za matumizi na wazazi wako, utawezaje kugharamia penzi lako?
Ikiwa umekwishamaliza masomo yako, na umri wako unaruhusu (zaidi ya 18), kipengele hiki hakikuhusu, maana penzi la dhati halizingatii fedha. Kama upo masomoni, basi yakupasa usome kwa bidii hadi utakapomaliza masomo yako, mapenzi yapo, utayakuta!

IPO DAWA!
Najua wengi watakuwa na maswali mengi, kwamba kwa sababu tu, mtu anasoma ndiyo asiwe na mpenzi? Au mwingine anawaza atawezeje kuishi bila kuwa na kampani ya jinsia tofauti? Hayo yote ni mawazo yenye maana kubwa katika mada hii. Wataalam wanawashauri wanafunzi kuwa mbali na mapenzi, kwa sababu mapenzi huteka hisia, muda mwingi huweza kuutumia kumuwaza mpenzi zaidi kuliko masomo, sasa kuna haja gani ya kuchanganya mambo wakati inawezekana kuacha?
Haikatazwi kuwa na rafiki wa jinsi tofauti na yako, lakini iwe kwa wema. Kuna mambo mengi unaweza kufanya na rafiki yako kuliko kuwa katika uhusiano wa kingono. Itapendeza kama mtasaidiana kimasomo au kuanzisha mijadala itakayowapa mwanga wa maisha yenu yajayo.
Pamoja na hayo, najua ni vigumu sana kuweza kudhibiti hisia, lakini hilo linawezekana kama utakuwa mtu wa mazoezi, msomaji wa vitabu mbalimbali vitakavyokujenga na mengineyo.
Mchukie kama rafiki yako wa kawaida, weka hisia za mapenzi pembeni, endelea na maisha yako na siku moja muda ukifika na ukiwa tayari utaingia katika uhusiano makini utakaokufurahisha siku zote za maisha yako.

MUHIMU
Katika vipengele vyote nilivyoanisha hapo juu, hasa katika kijisehemu cha kipato na masomo, haviwahusu wanafunzi wa vyuo! Hii inakuwaje? Kwa sababu wengi wao huwa ni watu wazima tayari, wenye ufahamu juu ya mambo mbalimbali ya maisha yao. Wanajua kupambanua mambo na wanajua wanachokifanya.
Wengine huwa tayari wapo katika ndoa au kuingia katika ndoa wakiwa vyuoni, hawa vipengele hivyo haviwahusu. Pamoja na hayo, angalia moyo wako unazungumza nini kabla ya kuingia katika uhusiano. Naamini nimeeleweka.
Tukutane hapa wiki ijayo kwa mada nyingine kali.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Thursday, May 10, 2012

USIFANYE SIMU IWE CHANZO CHA KUVUNJA NDO/MAHUSIANO

KAMA kawaida tumekutana kwenye kona yetu ili kujuzana mawili matatu kuhusiana na mahaba.
Nina imani mada yangu ya wiki iliyopita imezua maswali mengi kwa wapenzi juu ya upendo wa kweli ndani ya simu, wengine walifikia hatua ya kuyasema mengine juu ya matatizo ya simu katika uhusiano wao ambao ameingia shetani mvunja amani ndani ya nyumba.

Dada mmoja baada ya kusoma mada ya wiki iliyopita alisema simu ya mumewe imekuwa kama ngozi kwa laazizi wake huyo, kwani kila anapokwenda, hata iwe msalani. Anapobahatika kuipata anakuta ina ‘password’, kitu ambacho anaamini mume wake si muaminifu.

Aliniuliza kuwa mume wake kufanya vile inaashiria nini? Jibu lilikuwa jepesi, si mwanaume hata mwanamke ukiona simu yake ina password au anaichunga sana hata akiwa nyumbani, ujue pale hakuna uaminifu.
Kama nilivyoizungumzia simu wiki jana kuwa makusudia ya mtu aliyeitengeneza kusudio lake kubwa lilikuwa kurahisisha mawasiliano si kingine. Lakini wanadamu wenye mioyo dhaifu tumeitumia kama kichaka cha kuficha maovu yetu.

Sasa hivi ndani ya nyumba simu imekuwa chanzo cha kuvunjika kwa amani, asiye muaminifu uilinda simu yake kama ikulu ya Barack Obama.
Sasa hivi ndani ya nyumba zetu inaonyesha jinsi gani zimepoteza unaminifu kila mmoja analinda simu yake kuliko hata wivu kwa mwenzake.

Imekuwa kila mmoja anamwinda mwenzake alale ili aipekue simu, kwa vile ni mzoefu hata ukibahatika kuipata utakuta uchafu wake amefuta ili kupoteza ushahidi.
Ukiona hivyo mnakuwa mnaishi kwa mazoea lakini fahamu hakuna upendo ndani ya nyumba yenu na kuvunja ile ahadi ya kuishi kwa upendo na uaminifu katika ndoa.

Unaweka password unamuonyesha nini mwenzako? kama mwanaume unamuonyesha kabisa mkeo kwamba una wengine zaidi yake hapo unamfundisha nini mkeo, akilipa kisasi umlaumu nani?
Hebu turudie somo letu ambalo nimekuwa nikilitoa kila siku ili ambao hawakubahatika kusoma nilipolitoa ili tuangalie unachokifanya ni sahihi na ndiyo mapenzi?

Nilielezea mapenzi ni kupendana kuheshimiana kuoneana huruma kujaliana na uvumilivu.
Nilielezea mapenzi ni kupendana, kuheshimiana, kuoneana huruma, kujaliana na kuvumiliana. Ukiwa na mapenzi lazima utakuwa na vitu hivi kwa mwenzako, pia utakuwa muwazi kwake na mkweli ili kufanya muweze kuishi bila mmoja kuwa na mashaka na mwenzake.

Wapendanao siku zote hulinda heshima yao kwa kila mmoja kuilinda ya mwenzake, pia kuwa wawazi ili chochote kitakachokwenda kinyume, kiulizwe na kupatiwa majibu sahihi bila kujiumauma. Pia huwa hawana mipaka kuanzia katika miili yao na vitu vyote kwa vile huamini wao ni kitu kimoja, hivyo hawafichani kitu.
Watu kama hawa simu si chanzo cha matatizo, bali ni chombo cha mawasiliano, hakuna mtu wa kuificha simu yake wala kuweka password na kila mmoja ana uhuru wa kuishika au kuopokea ya mwenzake.

Nina imani somo langu limesomeka vizuri, sasa tunarudi kwenye mada ya leo kwa kuuliza swali, sifa nilizozieleza kuhusu mapenzi, je, wewe unazo au mwenzako anazo? Je, simu katika nyumba yenu inatumikaje? Ni chanzo cha migogoro au ni chombo cha mawasiliano ambacho kinaachwa popote bila masharti yoyote?

Tutumie simu kama chombo cha mawasiliano, hata kama si muaminifu katika uhusiano, si lazima mwenzako ajue jinsi gani unavyomdharau kupitia simu.

Simu isiwe chanzo cha migogoro na kuvunja nyumba zetu ambazo sasa hivi zimeingia mdudu ambaye ameonyesha jinsi gani tusivyo waaminifu, kitu ambacho kimeongeza ukosefu wa amani katika ndoa zetu.

Tuwe wawazi na wakweli kwa wenzetu, tuone aibu kuonyesha kwa vitendo sisi si waaminifu. Kama ulijua wazuri kuliko mwenzako wapo wengi, ulikaa naye kwa sababu gani?

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

NEW HIT:ibrah rush feat kalapina - serikali


TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

NEW HIT :marry me-rich mavoko


TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

NEW HIT:nuru-supastaa


TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

MJUKUU WA LUSIFA NAE KAJIUNGA NA FREE MASON?



Pray god kweka jina la stage. Baghdad ni msanii alieeanza mziki ki mazabe sana na kuonekana kupata bahati ya kupewa saport ya ghafla mara baada ya kupewa nafasi ya kuonyesha kipaji chake mwishoni mwa tamashaa la kutoa nafasi kwa vijana wanaochipukia kwenye mziki wa hip to hip hop ambalo lilizuriwa na wasanii wakubwa wa ndani na nje ya nchi kama fid q, langa, Saigon, na wasanii waliotoka nje ya nchi ni gnl zamba, na msanii kutoka nchini nijeria ambae jina lake halikuweza kupatikana na miongoni mwa waan dishi habari walioweza kuwepo kwenye tamasha hilo ni pamoja na fatma hasan, a.k.a fetty, ruben ndege a.k.a ncha kali ambae ni production manager wa clouds fm. Na kati ya maproducer wakongwe walionekana kuvutiwa na kipaji chake ni producer mkongwe ali baucha ambae aliweza kutoa ma mc wengi wakubwaa wa hip hop Tanzania kama fid q,rado, chidi benz, na wengine wengi. 


Na ndipo kukutanishwa na manyeko na kufanya ngoma yakie ya kwanza iliyoitwa hip hop imesimaama na kuweza kumfanya kuweza kujizolea mashabiki kibao kwa kuwa aliiachia siku moja baada ya kutolewa kwenye shindano la freestyl mc shujaa, ya mwaka 2009  iliyokuwa inaendeshwa na fetty chini ya kipindi cha bongo flavor.  Naukuaji wa mziki wake umekuwa wa ajabu ajabu kutokana kuwa mc wa kwanza Tanzania kufanikiwa kuwa na mashabiki wengi, kupiga shows nyingi kubwa, kufanya intaviews nyingi, kupewa promo na radio zote Tanzania bila kumbania ingawa mpaka alipofikia hana na hajawahi kuwa na manager wa aina yoyote na kila sehemu huwa anafanikiwa kufanya kazi bure na kujikuta wale wanaomfanyia kazi ndio kugaramika. Mfano baucha aliondoka na ngoma 5 na hakudaiwa hata shilingi 100 licha ya kutokuwa na makubaliano yoyote ya kusighn na studio ya baucha! Amefanya ngoma mbili ambazo zimefanya vizuri sana ndani na nje ya nchi full ng’ae ng’ae bila kutoa hat ash 50 kwa producer wa d fatality na hata baadae walipokuja kukorofishana aliweza kuja kufanya ngoma ya ohh mama na climax bibo, na wakati hawakuwa wakiongea na producer aliefanya mix bila malipo wakati messen alikiri ya kuwa ufanyaji kazi wake umebadilkika kwa sasa pesa mbele kama tai. Na kwa sasa anakabiliwa na kesi kubwa ya kutumia chater ya kundi alilokuwa akilitumikia mwanzoni mwa mwaka 2010 kabla ya kujitoa mwanzoni mwaka huu, na chaa ajabu uliwahi kusikia wapi mtu aliyepeleka kesi mahakamani kama mdai alietambulika kwa jina lililopo kwenye file la kesi dikison kuomba suluu baada ya kuhairishwa kesi mpaka tar 3 mwezi may. Hivyo hali yake ya kuwa anaogopewa na watui wengi lila sector. Inaweza kudhihirisha ya kuwa yeye ni muhusika wa familia ya freemason, kwa kuwa hajawahi kufanya shoe hata moja asiwe kati ya wasanii watatu bora kwenye show hiyo, na lazima ataonyesha vidole, au ishara yoyote ya ajabu. Baghdada, a.k.a notorious wa bongo, kwa sasa anatumia jibu la p.g kweka au mjukuu wa lusifer.


 Kuhusiana na mziki
Video yangu ya hip hop imesimama kunapicha ya fuvu, ukicheki kamba 2kamba kuna ishara za free mason, ukpitia baadhi ya lyn zake, mfano kwenye hip hap imesimama
     “ marehemu ninaeish kiufupi mi nmzmu
     Tanzania nw brnda  dar n bidhaa hadimu
      sijasomea majungu nawalasiujui umbea
     doubt nilipo sasa usiulize nilipotokea”
     kwenyengoma yake ya ng’aeng’ae alisema “nawauzunisha waliojipaga kuelekea moton nawa furaisha wenye tv yakuona pepon kwenye ooh mama  “yee ni zombie joo mzimu wamrehem huwa hauzirai” kwenye kamba 2 kamba aliziirisha zahili kuwa anatoa kafara kwa kunywa damu zawatu kwa kusema “damu za dadazao zinatolewa kafara ghetto” licha ya ngoma mpaya  ambayo ukisikiliza lyn moja baada ya moja  kumuusisha na freemason kwa kukiri kuwa yeye ni mjukuu wa Lucifer jina la kiongozi wa free mason!  Na moja ya line zake anasema was bon freemason na ubongo alipewa na lusifer, been haso kutafuta damu awe satisfai. Na ukiisikiliza mwishoni mwa ngoma hii utasikia akisema diss line kwa dimond platinum na huwezi amini kwa msanii mkubwa kama diamond ambae ukionekana kugusa hata kiatu chako kwa soli yako haoni shida kukufungulia kesi ila im ekuwaje kuwa kimya kwa kauli hiii kutokuifanyia kazi!






TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

IT'S ABOUT TIME! MISS DAR CITY CENTRE 2012 IS AROUND THE CORNER GET READY...!!!


TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

FAIDA YA KUFANYA KAZI AU SHUGULI INAYODHARAULIWA.....


BINADAMU wengi wana tabia ya kuchagua vitu na hasa vizuri kwa lengo la kulinda heshima yao mbele ya wenzao. Kwa tabia hiyo ya utukufu wengi wetu tunapenda kuwa na kazi nzuri si itakayotusaidia kuishi bali kukidhi heshima yetu mbele ya jamii.
Vijana wengi waishio hasa maeneo ya mijini wako radhi kuishi maisha ya kubangaiza kwa kukaa vijiweni kupiga soga na kuvuta bangi lakini si kwenda kuuza mboga za mitaani, kubeba zege kwenye kandarasi za ujenzi au kuuza maji kwenye mikokoteni.

Hawataki kazi au shughuli zinazochukuliwa kama fedheha licha ya kwamba wanaozifanya wanajipatia kipato cha kuendesha maisha yao na familia zao kwa sababu tu ya ule umwinyi mkuu wa kutaka utajo mzuri mbele za watu.
Nayasema haya kwa sababu miaka michache tu iliyop ita mimi pia niliishi kwenye utumwa huu wa utukufu, nilijiona siwezi kufanya kazi dhaifu hata kama zina kipato, kwa fikra tu kwamba akiniona msichana fulani pale mtaani atanidharau. Kumbe kwa upande mwingine nilidharaulika zaidi kuliko hata nilivyojikinga kwa kukwepa kazi.

Kwa namna yoyote ile, heshima ya mtu ni kazi na mafanikio ndiyo kipimo cha akili. Hii haijalishi unafanya shughuli ya heshima kimtazamo au yenye kudharauliwa na wengi kimawazo.
Haiwezi kutokea kijana muuza maji aliyejenga nyumba yake ya vyumba vitatu na kujiendeshea maisha yake akadharauliwa na mfanyakazi wa benki anayetangatanga kwa ufujaji wa fedha na kukosa tija ya maisha, akaheshimiwa kwa lemba la kazi yake tu. Kamwe hilo haliwezekani.

Ikiwa ni hivyo, kwa nini watu wanachagua kazi? Je, hatuna ushuhuda wa mafundi viatu kuwa na nyumba, miradi na biashara kubwa huku wafanyakazi maofisini wakigeuka wakopaji kwenye maduka ya Wamachinga wanaotembeza nguo mikononi kwenye mitaa ya mijini? Naamini ushahidi upo wa kutosha.

Maeneo mengi ya wakulima wa zao la tumbaku katika mkoa wa Tabora, kwa mfano, na vijana wanaomiliki maduka madogomadogo maarufu kama vioski ni wageni ambao walifika kwenye mkoa huo kama watumishi au wasaidizi wa mashambani, wakifanya kazi dhaifu ambazo wenyewe huzitafsiri kama shughuli zisizokuwa na heshima. Lakini pato la kazi hizohizo ndilo hatimaye huwapatia vioski ambavyo wenyeji huenda kukopa bidhaa.

Katika hali ya kawaida, kazi zinazoonekana dhaifu ni funzo kubwa sana katika maisha na mara nyingi hujenga ari ya aina yake katika uwajibikaji wenye lengo la kujikomboa na hiyo zana ya kudharaulika.
Watu wengi matajiri historia zao huanzia kwenye kazi dhaifu. Huko ndiko kulikowafunza nidhamu ya matumizi ya fedha. Kwenye dharau kumejaa maarifa na mbinu za ukombozi kuliko mahali penye maisha ya heshima ambako hupumbaza na kuwafanya wahusika wasipige mbio kuelekea kwenye mafanikio zaidi.

Wito wangu kwa vijana wenzangu, Watanzania wote, tusikubali kuishi na ufalme, heshima na utukufu usioweza kutusaidia, badala yake tukubali kufanya kazi hata zinazoonekana dhaifu kwa lengo la kujipatia kipato ili hatimaye tutafsri hali ya kudharauliwa kuwa heshima.


TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

JE UNAZIJUA HIZI ''I LOVE YOU'' ''I MISS YOU'' ZA KICHINA? SOMA HAPA UJUE JINSI YA KUDEAL NAZO......

Nazungumzia mapenzi ya ‘Kichina’ ambayo sasa hivi yamekuwa kama fasheni.
Mapenzi ni mhimili muhimu sana katika maisha ya binadamu. Mtu asiyeyapa maanani, huyo ana kasoro zake na kamwe hawezi kuyafurahia maisha.
Mapenzi hasa unapofanikiwa kumpata mtu sahihi, yana raha yake. Unaweza kujikuta unanenepa tu kutokana na kuwa na mtu anayeonesha mapenzi ya kweli kwako, kukujali na kukuthamini katika shida na raha.
Hata hivyo, mapenzi ya sasa yamebadilika sana, yamekuwa ni tofauti na yale yaliyokuwepo enzi za mababu zetu. Siku hizi hakuna mapenzi, usanii na ulaghai vimetawala kiasi kwamba akitokea mtu akakuambia anakupenda huwezi kumuamini mara moja.

Kwa nini mada hii?
Rafiki yangu ambaye siwezi kumuanika hapa kwa sasa yupo kwenye penzi la kuibiwa. Mpenzi wake ambaye walikuwa na malengo ya kuoana kamfanyia kitu ambacho kimeniuma licha ya kwamba siye niliyetendwa. Nilikuwa nikiwaona jinsi wanavyopendana kwa dhati, hakukuwa na mazingira ya unafiki kabisa.
Kila mmoja alijitahidi kuonesha upendo wake kwa mwenzie kiasi kwamba penzi lao mara kwa mara nilikuwa nikilichukulia kama mfano wa kuigwa. Hizi I love you, I miss you zilikuwa hazikauki kwao. Yote tisa, wapenzi hawa walikuwa wakiaminiana sana, yaani kila mmoja aliamini mwenzake hawezi kumsaliti.
Kilichotokea juzi ndicho kilichonisukuma kuandika makala haya na hapo ndipo utajua mapenzi ya sasa asilimia kubwa ni ya Kichina. Wakati rafiki yangu kasafiri, mimi kwa macho yangu nilimshuhudia yule dada akiingia gesti na mwanaume mwingine. Niliumia sana kana kwamba mimi ndiye niliyekuwa nimesalitiwa.
Hata hivyo, sikutaka kuwa chanzo cha wawili hao kuachana, nikabaki na siri yangu moyoni mpaka leo. Kinachoniumiza zaidi ni kwamba, yule jamaa karudi na mapenzi yao yako vile vile. Jamaa anajisifia kuwa anapendwa lakini kumbe mapenzi ni ya Kichina.

Tunajifunza nini?
Usanii katika mapenzi sasa unachukua nafasi kubwa sana. Dada zetu wengi wao wako kifedha zaidi. Unamkuta anajifanya kukupenda sana kumbe hakuna chochote, wizi mtupu!
Wanaume nao usiseme, si ajabu ukamkuta akionesha mapenzi ya ajabu kwa msichana na kufikia hatua ya kuahidi ndoa lakini kumbe lengo lake ni kuonja penzi kisha akimbie.
Jamani, tunatakiwa kuwa makini sana tunapoingia kwenye uhusiano. Ni vigumu kumjua mtu mwenye mapenzi ya dhati kwako lakini unapokuwa na mtu ambaye hizi I love you, I miss you hazikauki, jaribu kumchunguza kwani huenda ni tapeli wa mapenzi.
Maneno siyo vitendo
Haya maneno ambayo hutolewa na watu wenye mapenzi ya dhati sasa hivi imekuwa ni tofauti. Unaweza kuitwa majina yote matamu, mara dear, my sweetheart, my love lakini kumbe anayekuambia anasema tu na wala hamaanishi kwamba yanatoka moyoni mwake.
Usiwe mbumbumbu na kudatishwa na maneno, kama kweli anakupenda vitendo vyake ndivyo vifanye kazi na siyo kulainishwa na ‘vijineno’ tena vya Kiingereza ambavyo yeyote anaweza kukuambia na wala asimaanishe hicho anachokisema.

Kwa leo, naomba niishie hapo nikiamini sasa utakuwa makini kuhakikisha hauingii kwenye penzi la Kichina......
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Wednesday, May 9, 2012

UMRI, MAJINA YA LULU YAZUA UTATA MAHAKAMANI

UTATA kuhusu umri wa mtuhumiwa wa kesi ya mauaji, mwigizaji wa filamu nchini, Elizabeth Michael ‘Lulu’ leo umeanza kutoa matokeo, kwenye ya Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu, Dar es Salaam, huku kesi yake ikipigwa tena kalenda hadi Mei 21, mwaka huu.
Lulu anayekabiliwa na kesi ya kumuua mwigizaji mwenzake, Steven Charles Kanumba, kwa sasa anasema ana miaka 17, lakini katika mahojiano kwenye kipindi cha TV cha Mikasi, kabla ya kifo cha The Great aliwahi kusema ana umri wa miaka 18.
Wakili wa mwigizaji huyo aliyekulia kwenye sanaa hiyo kuanzia akiwa kinda katika kundi la Kaole Sanaa la Magomeni pamoja na marehemu Kanumba, Kenned Fungamtama leo aliwasilisha ombi katika Mahakama hiyo, akiitaka iitupilie mbali kesi hiyo ili ikafunguliwe upya katika Mahakama ya Watoto, akidai Lulu ana umri chini ya miaka 18.
Lakini Wakili Mwandamizi wa Serikali, Elizabeth Kaganda alipinga akisema suala hilo, inabidi kwanza lifanyiwe uchunguzi na vyombo vya dola ili kugundua ukweli kuhusu umri wa Lulu(pichani kushoto).
Akizungumza mahakamani hapo, Wakili Kaganda alisema mbali na umri wa Lulu kuwa na utata, lakini hata jina lake halisi nalo ni tatizo, pia kwani wakati wengi wanamfahamu kama Elizabeth Michael, lakini cheti chake cha kuzaliwa kinasomeka Diana Elizabeth.
 
Katika ufafanuzi wake, Hakimu Mkazi, Augustina Mmbando alisema analitupilia mbali ombi la upande wa utetezi, kwa sababu mtuhumiwa anakabiliwa na kesi ya mauji na imefunguliwa chini ya Kifungu cha 196 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2002.
Alisema kwa mujibu wa kesi hiyo, Mahakama yake haina mamlaka ya kuisikiliza kesi hiyo, zaidi ya Mahakama Kuu. Hakimu Mmbando ameiahirisha kesi hiyo hadi Mei 21, mwaka huu.
Tayari msisimko wa kesi hiyo unaonekana kuanza kupungua taratibu, kwani leo Lulu aliwasilishwa katika ulinzi wa kawaida na mahakamani hapo hakukuwa na idadi kubwa ya watu, kama ilivyokuwa alipofikishwa mahakamani mara ya pili, mwezi uliopita.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

RIHANNA REVEALS SKETCHES FOR HER 2ND EMPORIO ARMANI CAPSULE COLLECTION...!!!


RiRi has revealed sketches for her second collection with Italian label Emporio Armani, and put her signature twist on it. 

The singer’s exclusive collection includes a denim boiler suit, slouchy shirts and a leather jacket. With her infamous initial on an over sized bag, the collection is set to be a sure fire hit.

The star recently revealed in an interview with Ryan Seacrest that, ‘I want people toreally trust me before I just say “Buy it because it’s mine.”‘ She has also expressed that one day she’d love to have her own clothing line, after her first collaboration was such a huge success.


 Can’t wait to see the line, if it’s anything like her own unique style I know we’ll love it!

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

ALBINO MODEL DIANDRA FORREST ROCKS CAKE MAGAZINE ISSUE 4...!!!

Model: Diandra Forrest
Photographer: David Urbanke for Cake Magazine #4
Styling: Jordan Bradfield and Jaime Kreindler
Makeup: Victor Henao
Hair: Cesar Ramirez
Source: Fashion Bomb Daily
Source: Cake Magazine

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

MSANII SAJUKI KUELEKEA NCHINI INDIA JUMAPILI HII & MAPEMA WIKI IJAYO KWA AJILI YA MATIBABU ...!!!

MSANII wa filamu nchini Sadiki Juma Kilowoko (Sajuki) anatarajiwa kusafirishwa kuelekea nchini India mapema wiki ijayo au Jumapili hii kwa ajili ya matibabu. 


Akizungumza na mtandao huu mke wa Sajuki - Wastara Juma amesema kwamba baada ya kukamilika kwa asilimia kubwa ya michango ambapo wameweza kupata jumla ya Sh milion 16 pamoja na ticketi tatau za ndege zilizotolewa na wasanii na wadau mbalimbali wa ndani na nje ya nchi walio guswa na ugonjwa wa msanii huyo, yeye pamoja na mtu mwingine mmoja wataondoka na Sajuki kuelekea nchini India ambako Sajuki ataenda kuanza matibabu.

Rais wa Shirikishio la Wasanii nchini Ndugu Simon Mwakifamba amesema kuwa fedha hizo zitasaidia kwa kuanzia maana jumla ya fedha iliyo kuwa inahitajika ni Sh milioni 25 na kuongeza kuwa michango mingine inazidi kuchangishwa na pesa hizo zitatumwa kwa ajili ya kuendelea na matibabu zaidi. 

Sajuki anasumbuliwa na tatizo la uvimbe tumboni. Tuendelee kumuombea Sajuki pamoja na familia yake.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

new track released kutoka *B~ONE~RECORDS* chini ya producer *KID~MONEY* artist wa B~ONE~RECORDS P-MONEY akimshirikisha msanii alieshinda KILI STAR SEARCH dodoma DUBSONN have fun..


TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
 

for more information call us

+255718953088
-------or-------
+255784953088
*email*
innocentfabian@gmail.com
THANKS

quote of the day

"Don't criticize me simply because I am different. Understand me, and you will most likely appreciate my difference and criticize your variance."