Social Icons

Monday, June 25, 2012

KWA AMBAO HAMJAONA PICHA ZA YALIYOJIRI KWENYE UZINDUZI WA FILAMU MPYA YA WEMA

                                                           Omotola akiwa na mwenyeji wake Wema 
                                          Miriam Odemba, Omotola na Mange mamaa wa U-Turn!!
                                                                    Omotola akifurahia na kucheza ngoma iliyoandaliwa mahsusi kwa mapokezi yake  KWA PICHA ZAIDI NA MENGI YALIYOJIRI USIKU HUO GONGA HAPO CHINI.


                       YALIYOJIRI KWENYE UZINDUZI WA FILAMU MPYA YA WEMA ...  


                                          Habari na Picha Shukrani kwa BONGO STAR LINK



Enjoy!!

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Monday, June 11, 2012

PICHA 20 ZA NYUMBA MPYA ANAYOISHI MWIGIZAJI WEMA SEPETU.

                                                          gonga hapa kea picha zaidi

             PICHA 20 ZA NYUMBA MPYA ANAYOISHI MWIGIZAJI WEMA SEPETU.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Friday, June 8, 2012

Mbinu za kuwashawishi watu wakusaidie

WATU wengi tunapokuwa kwenye mikwamo huwa tunatamani sana kuona wenzetu wanatusaidia. Yawezekana hata unaposoma makala haya kuna mambo unahisi unahitaji msaada kutoka kwa binadamu wenzako lakini hao unaotaraji wakusaidie inaonekana kama wamekupa kisogo.
Katika kazi yangu ya ushauri wa masuala ya Elimu ya Ufahamu na Nafsi nimekuwa nikikutana na watu wengi wenye matatizo makubwa ambayo kusema kweli yanahitaji msaada wa wasamaria na wakati mwingine hata kutoka kwa bosi kazini au ndugu waliofanikiwa.
“Huu ni mwaka wa tatu sijapata kazi nahangaika na mwanangu, ndugu zangu wana uwezo lakini hawataki kunisaidia.”Aliniambia dada mmoja hivi karibuni ambaye naamini maelezo yake yalinipa mwanga wa kuandika makala haya kwa sababu niliamini ndugu na jamaa wanaoweza kumsaidia dada yule wapo lakini hajui namna ya kuwavutia.
Katika hali ya kawaida matokeo yoyote tunayoyaona kwenye ulimwengu huu yawe ya kisayansi au kijamii yamevutwa kupitia matendo, fikra na vichocheo vingine. Nyumba hazioti kama uyonga zinajengwa, magari yanategenezwa na watu na hata tabia nazo kuna vitu vya kufanya mpaka kumfanya mwanadamu awe na akili, apendwe au atajirike.
Kwenye maisha kuna kitu kingine muhimu ambacho kinaendana na falsafa ya kuvuta vitu nacho ni kutengeneza mkondo wa maisha. Huwezi kupata fedha mpaka utengeneze mkondo ambao fedha hizo zitapita, inaweza kuwa mkondo wa kuuza bidhaa, kufanya kazi nakadhalika.
Lakini pia ukitaka umeme lazima uweke mkondo wa nyaya, kwenye maji utatakiwa kutandaza bomba ili kipite kile unachotaka kipite kupitia mtandao huo.
Swali langu kwa yule dada aliyenisimulia matatizo yake lilikuwa ni “umetengeza mkondo wa kusaidiwa, unajua namna ya kumvuta mtu akusaidie?” Kusema kweli alishangaa nilipomuuliza swali hilo, yawezekana hata wewe msomaji wangu unashangaa, unawezaje kumvutia mtu akusaidie?
Jibu la swali hili ni rahisi na bila shaka hii ndiyo mbinu pekee ya kumfanya mtu akusaidie haraka nayo ni kumsaidia yeye kwanza kabla hajakusaidia.
Umsaidie nini wakati wewe huna kitu? Ni vema kutambua kuwa kila mwanadamu anahitaji msaada wa wengine, kuna watu wenye fedha nyingi lakini wanahitaji msaada wa heshima, akitokea mtu akiwapa heshima hufurahi na kutoa walivyonavyo kama asante ya heshima.
Mbali na hao wanaotaka msaada wa heshima wapo ambao wanapenda sana mtu wa kuwapelekea watoto shule, kusimamia miradi vizuri, kufagia nyumba zao, kufuliwa nguo, kuzinyoosha, kutumwa hiki na kile kwa uaminifu mambo ambayo anayehitaji msaada anaweza kusaidia bure lakini baadaye akalipwa anachotaka.
Kama hilo halitoshi mtu anaweza kutoa muda wake kazini kwa kufanya kazi za ziada bila malipo, lengo likiwa ni lilelile la kumfanya bosi wake ahisi uwepo wake kwenye ajira ni msaada na hivyo kuwa tayari yeye pia kusaidia kupitia mkopo, nyongeza ya mshahara, safari na semina ambazo zitasaidia kuongeza kipato.
Kwa somo hili, naamini tunaohitaji kusaidiwa tutakuwa tumefahamu namna ya kuvuta misaada na hivyo kutumia mbinu hii kujipatia mahitaji yetu.
Nashukuru kwa kuwa pamoja nami!
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Unafahamu kwa nini watu wanakudharau? Soma hapa

HAKUNA kitu kibaya maishani kama kuonekana upo katika daraja la chini na mtu wa kudharaulika kwenye jamii unayoishi. Kisaikolojia kuna madhara makubwa.
Ni imani yangu kuwa kila mwanadamu timamu anapenda kuheshimiwa lakini wengi wetu tunashindwa kupata heshima tunayoitaka kwa sababu hatufahamu jinsi ya kuishi mbele ya wenzetu.
Kitaalamu, hakuna jambo ambalo hutokea maishani bila sababu maalumu hivyo hata kudharauliwa kwako au kwetu ndani ya jamii tunayoishi kunatokana na jinsi tunavyoenenda.
Mwalimu wangu wa somo la maisha na saikolojia, Eric Shigongo, aliwahi kuniambia ‘Nothing happens in the sky, but the elements should be there,’ akimaanisha kuwa hakuna kitokeacho angani pasipo kuwa na dalili au sababu zake.
Naomba nianze kutoa njia za kukusaidia kurejesha heshima yako kwa kuperuzi na wewe baadhi ya dokezo muhimu zinazoweza kukusaidia kujitambua na kuweza kuyaepuka maisha ya kudharauliwa.
MUONEKANO
Kwanza kabisa ni jinsi unavyoonekana. Muonekano ninaouzungumzia hapa ni usafi wa mavazi na mwili kwa ujumla. Hata siku moja hakuna mchafu anayeheshimika katika jamii anayoishi hata kama ana kipaji kikubwa kiasi gani.
Kwa hiyo uchafu wa mavazi na mwili huchangia mtu kudharauliwa katika jamii anayoishi. Linaweza kuwa jambo dogo sana lakini ni moja kati ya sababu kubwa inayochangia kuporomoka kwa thamani yako mbele ya wenzako.
MAZUNGUMZO
Hapa naomba nieleweke kuwa unachokizungumza kinaweza kukujengea heshima au kukubomolea heshima. Kauli zisizo na busara zitakufanya udharaulike kwa kila mtu. Uropokaji usiokuwa na mantiki huchangia kuporomosha heshima yako hasa kama utakuwa muongeaji zaidi. Biblia inasema penye wingi wa maneno hapakosi uovu.
UTENDAKAZI WAKO
Ndugu zangu, siku zote heshima ya mtu ni kazi. Watu wengi hawapendi kufanya kazi kwa bidii huku wengine wakijiendekeza kwa tabia ya kuombaomba, jambo hilo halifai kwa vile huchangia kubomoa heshima yako mbele ya jamii. Fanya kazi usiishi bila kujishughulisha.
KUTOTIMIZA AHADI
Kama una tabia za kuahidi mambo halafu unashindwa kuyatekeleza, basi unajiweka katika nafasi mbaya ya kutunza heshima yako katika jamii unayoishi. Bora ukwepe kutoa ahadi kuliko kuahidi na kutotimiza.
SIFA ZISIZO NA MAANA
Nakumbuka msemo mmoja kutoka kwa mwandishi mwandamizi aliyekuwa mtaalamu wa falsafa za maisha, marehemu Adolf Balingilaki, ambao unasema kwamba:
“Ukitafuta heshima kwa gharama ya juu, basi utalipwa dharau kwa bei nafuu.”
Msemo huu unamaanisha nini? Siku zote ukiwa unafanya mambo yako kwa ajili ya kusifiwa au mazungumzo yako kuwa ya kujiinua, watu watakudharau.
KUTOKUWA MWAMINIFU
Suala la uaminifu ni pana, kuna uaminifu wa fedha, siri, dhamana na mambo kama hayo, hivyo ni vema kila unachoaminiwa lazima ukitunze kwani ukiwa mtu wa kuvunja uaminifu fahamu kuwa utashusha heshima yako.
Kwa leo naomba niishie hapa, ukiwa na swali au maoni nitafute kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook au tembelea blogu yangu ya www.richamanyota.blogspot.com kwa elimu zaidi ya kisaikolojia. Asante kwa kunisoma.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

DJ FETTY TO ROCK THE BIG BROTHER STARGAME PARTY THIS WEEKEND...!!!

Dj wa kwanza wa kike nchini Tanzania Fatma Hassan aka Dj Fetty wa Clouds Fm amepewa heshima ya kuwa Dj wa kwanza wa kike kutoka Afrika Mashariki kutumbuiza kwenye mashindano ya Big Brother Africa.

Kupitia ukurasa wake wa Facebook Fetty amesema, “Juma mosi hii na jumapili nitakua nikispin ndani ya Jumba la BBA STARGAME, nitume kwa kuniandikia playlist itakayo wapagawisha…na shinda very nice cape ya big brother na high quality Tshirt kutoka CloudsFm…legoooooo.”

Fetty ambaye kwa muda alikuwa amepumzika shughuli za udj na kuendelea na utangazaji wa kawaida, amesema imemlazimu kujifua tena ili kuhakikisha kuwa ‘haangushi maembe’ (kumix vibaya nyimbo) wakati atakapokuwa akipiga ngoma.
Amesema mwaliko huo ameupata katikati ya mwezi May na tangu hapo amekuwa akijikumbushia ujuzi kwenye ‘wheels of steel’ kwakuwa hiyo ni nafasi kubwa inayohitaji maandalizi ya kutosha.
Mwaka jana Dj wa kike kutoka kituo cha radio cha YFM cha Ghana Nana Kessewa Adu aka DJ Kess alialikwa pia kuburudisha kwenye Big Brother Amplified.
Hiyo si mara ya kwanza kwa Dj wa Clouds FM kupata mwaliko huo. Mwaka jana Dj Steve B naye alipewa fursa hiyo ya kuonesha ujuzi wa mikono yake kwenye 1 and 2!

---
Two weeks after Bongo Flava artiste Diamond thrilled fans on reality TV show BBA, another Tanzanian entertainer DJ Fetty will this weekend entertain housemates at Big Brother House.

Apart from the Saturday Night party, she will also perform at the nomination/eviction party on Sunday.

DJ Fetty who plies her trade with local radio station Clouds Fm in Dar-es-Salaam is considered as one of the best female DJs in the country.

She first rose to prominence while presenting a popular afternoon show (Dr Beat) before she joined a disk jockeying group Nyuki DJs in a show at the time known as Saturday night live.

DKB, Zainab leave BBA
Johannesburg.  After two successive seasons that saw Hannington in 2010 and lotus in 2011 being evicted from the BBA house because of violence, this year’s contestants became the latest victim.

Ghana’s DKB and Sierra Leone’s Zainab became the latest victims to face Biggie’s wrath as they failed to desist from violence which is against BBA rules.

The sending off of the contestants brought the number of housemates to seven in five days after Esperanza and Seydou decided to back out of the Stargame contest. 

Source: Bongo5 & The Citizen
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

UNAPENDWA, UNAACHWA TATIZO NI NINI?-2

KUJUA sababu ya tatizo angalau ni mwanzo wa kuelekea kwenye utatuzi, maana unakuwa umeshafahamu kwa nini jambo fulani linalotokea katika maisha yako. Marafiki zangu, kuachwa ni tatizo kubwa sana katika mapenzi.
Linaumiza sana. Linachoma na kuwanyima raha wahusika. Sikia nikuambie kitu kimoja, kuumia moyoni peke yake hakutoshi kukuondoa kwenye tatizo. Lazima ujiulize, kwa nini unaachwa? Hapo utakuwa katika nafasi nzuri ya kuhakikisha unaondoka katika utumwa huo.
Ndiyo shabaha hasa ya mada hii. Wiki iliyopita nilianza kwa dondoo tatu, leo tunaingia katika hatua ya mwisho. Karibuni darasani marafiki.
UNASHAURIKA?
Tabia ya kung’ang’ania mambo ambayo mpenzi wako hapendi ni kati ya sababu zinazotosha kabisa kukufanya uachike. Inawezekana mpenzi hapendi aina fulani ya mavazi, tabia fulani mbaya na amekuambia kwa nini hapendi lakini wewe ukaendelea kung’ang’ania. Hili ni tatizo.
Acha uking’ang’anizi, jaribu kuwa muelewa. Mwenzi wako anapokataa kitu na kukueleza sababu za msingi, msikilize na kama unaona anachokuambia hakifai basi mjibu kwa hoja na siyo kumuwekea kiburi.
DHARAU
Wanawake wenye dharau wapo katika nafasi kubwa zaidi ya kuachwa na wapenzi wao. Utakuta mwingine dharau zake zinazidi mipaka mpaka kwa ndugu wa mpenzi wake. Wakigombana kidogo, anaweza kutaja hata wazazi au ndugu wa karibu na mpenzi wake.
Ni mwanaume gani anayependa kuishi na mwanamke mwenye mdomo mchafu? Mwenye dharau? Anayeamini kila kitu anaweza mwenyewe? Sifa ya kwanza ya mwanamke ni heshima, kama mwanamke huna heshima basi fahamu kwamba huwezi kuishi na mwanaume hata siku moja.
Katika maisha ya ndoa kati ya mambo ya msingi ambayo huzingatiwa na wengi ni pamoja na kila mmoja kukubalika na ndugu wa pande zote, sasa itawezekana vipi wewe kuolewa ikiwa hata hao ndugu wenyewe unawadharau? Unawadhalilisha kwa maneno makali? Itawezekana vipi?
Mwanamke lazima uwe na heshima, uwe na haiba ya kike, siyo unaishi mradi siku zinakwenda. Kama huwa unaachwa kila wakati, chunguza tabia hii nayo inaweza kuwa chanzo cha wewe kuachwa!
UNAITAMBUA NAFASI YAKO?
Baadhi ya wanawake huwa hawataki kutambua na kutumikia nafasi zao, mwanamke hawezi kuwa sawa na mwanaume kwa kila kitu. Hata kama kwa bahati mbaya mmetofautina, kama mwanamke ambaye anatarajiwa mpenzi wako aje kuwa ‘kichwa cha nyumba’ yako, lazima uonyeshe unyenyekevu.
Tulia, msikilize kwa makini, hata kama ni yeye amekosea, usitumie kauli chafu ambazo zitamuudhi. Zungumza naye kwa staha ukitambua nafasi yake. Wakati mwingine wanawake wenyewe wanasababisha waachike. Usikubali kuwa hivyo!
KURUDIA MAKOSA
Hakuna binadamu ambaye hakosei. Inaelezwa kwamba, kukosea ni sehemu ya ukamilifu wa mtu. Mwanasaikolojia mmoja aliwahi kusema: “Ni vizuri watu wakosee ili wajifunze, huwezi kujua kitu bila kukosea, lakini unaruhusiwa kukosea mara moja tu!”
Kama ukichambua neno moja baada ya lingine la Mwanasaikolojia huyo, utaweza kuona jinsi sentesi yake fupi ilivyo na maana kubwa. Kwa mantiki hiyo hata kama utakosea mara mia moja, hakuna tatizo, lakini yawe makosa mapya. Kosea kila siku, lakini kitu kipya, hii inamaanisha kwamba, kwa sababu kukosea ni kujifunza, basi kama utakosea mara mia, utakuwa umejifunza pia mara mia moja. Upo hapo?
Sasa wanaume wengi hawapendi wanawake ambao wanakosea na kusahau! Jenga utaratibu wa kuheshimu unachoambiwa; Ukielezwa hakifai, usikaidi, huna sababu ya kurudia tena.
Kurudia kwako mara nyingi ni kuzidi kumkera mwezi wako ambaye lengo lako hasa ni kuishi naye hapo baadaye.
BADILIKA
Kama hayo yote hapo juu yanakuhusu ni wazi kwamba unatakiwa kufanya mabadiliko ya haraka sana katika maisha yako, kama ni kweli unataka kuolewa. Siyo rahisi mwanaume ambaye anatafuta mke akakubali kuwa katika uhusiano na mwanamke mwenye tabia zako.
Anza taratibu, rekebisha moja baada ya lingine, halafu kuwa makini katika kila jambo, mwisho wake utakuwa kwenye nafasi nzuri ya kupata mwenzi wa maisha. Naamini somo limeeleweka, hadi wiki ijayo kwa mada nyingine, USIKOSE!
Joseph Shaluwa ni Mshauri wa Mambo ya Mapenzi anayeandikia magazeti ya Global Publishers, ameandika vitabu vya True Love, Let’s Talk About Love na Who is Your Valentine? vilivyopo mitaani.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

UNAPENDWA, UNAACHWA TATIZO NI NINI?

KUACHWA au kuachana kwa wapenzi si jambo la ajabu sana katika jamii, lakini inapotokea wewe unakuwa wa kuachwa kila siku, hapo ndipo kwenye tatizo. Ndiyo zao la mada hii. Kwa nini uingie kwenye uhusiano na kuachwa kila mara?
Msingi wa mada hii ni wanawake, ingawa hata wanaume kuna wakati wanaachwa na wenzi wao. Rafiki zangu, pamoja na ugumu wa jambo hili, lakini inakupasa ukubali kwamba wewe ni tatizo.
Kuufanya ubongo wako kukubali kuwa wewe ni tatizo, utakuwa mwanzo mzuri wa kutafuta dawa. Ni jambo gumu kidogo kupata hekima ya kugundua jambo hili, lakini waliobahatika wanafanya maamuzi ambayo hayawaumizi mioyo yao.
Haya mambo yanawezekana rafiki zangu. Kwanza ni kukubali kujifunza, kuangalia wapi ulikosea, ni kipindi gani wenzi unaochana nao wanapatwa zaidi na hisia za kukuacha n.k. Baada ya hapo ni rahisi kusogea mbele zaidi katika kujua jinsi ya kutatua tatizo ulilonalo.
Wapo wanawake wengi sana ambao wanahangaika kwa sababu ya kuachwa kila siku. Kila mwanaume anayekuwa naye, baada ya muda mfupi tu, anamuacha! Hajui tatizo, badala yake anaishia kulia tu. Kulia kwako hakutakusaidia lolote kama hutakaa chini na kujiuliza ni wapi kwenye matatizo, ni sehemu gani huwa unakosea.
Una miaka ishirini na nne tu, lakini umeshakuwa na wanaume tisa! Hili ni tatizo, tena kubwa ambalo linahitaji dawa ya kuponya na siyo ya kutuliza maumivu. Twende darasani...
KUJIRAHISISHA...
Kwanza jaribu kujichunguza kama una tabia ya kujirahisisha. Ni kweli umekuwa na tabia ya kujishusha thamani na kuona kama wewe ni kuonewa? Kuchezewa? Mwanaume mwenye ndoto na mwanamke wa baadaye wa maisha yake hahitaji mwanamke wa aina hii.
Anapenda zaidi awe na mwanamke mwenye msimamo anayetambua thamani yake yeye mwenyewe na maisha yake kwa ujumla. Hapendi mwanamke mwepesi kuingilika. Kama utakuwa wa aina hii, hata kama atakuwa amekupenda, ataishia kukutumia na kukuacha, kwani wewe mwenyewe umejionesha wa namna hiyo.
Mwanaume anapenda mwanamke wa kumsumbua kidogo, angalau baadaye apate stori za kusema; “Lakini mama nanilii ulinisumbua!”
Huu ni ukweli ambao baadhi ya watu wanaukwepa. Acha kujirahisisha. Kujirahisisha huku ni pamoja na suala zima la kufanya mapenzi. Usiwe na haraka na tendo hilo, usiulizie juu ya kufanya mapenzi, lakini kama ikitokea jamaa akataka, usikubali haraka. Onyesha msimamo wako, ukiainisha usivyotaka kuchezewa.
JICHUNGUZE MWENYEWE
Wakati mwingine mambo yako yasiyotamanika yanaweza kuwa chanzo cha wewe kuachwa na wenzi wako kila wakati. Angalia tabia zako, tizama mienendo yako, marafiki, kauli na kila kitu ambacho unadhani kinaweza kuwa tatizo.
Mwanaume hapendi kuwa na mwanamke ambaye ana kampani mbaya, kwani anaamini na wewe pia inawezekana ukawa na tabia chafu kama rafiki zako, lakini kauli nzuri kwa mwenzi pia ni kati ya mambo ambayo mwanaume mwenye nia ya kuoa atavutiwa navyo. Jichunguze!
VIPI, UNAJALI?
Kujiona wewe ni bora kuliko wanawake wote hakukusaidii, sana sana kunazidi kukurudisha kwenye matatizo yale yale kila siku. Mwanamke ambaye hajali na haoneshi umakini wakati akizungumza na mpenzi wake, hana sifa ya kuwa mke.
Kama ni kweli unataka kuwa mke, lazima uwe makini, uoneshe kujali kwako na kumuona mwenzi wako kila kitu. Mheshimu, mpe nafasi ya kwanza, hiyo inaweza kuwa safari nzuri ya kuelekea kwenye mafakio.
Jifunze unyenyekevu, ukikosea kuwa wa kwanza kuomba msamaha, kubali kusamehe na hakikisha kwamba unakubali kufundishwa unapokosea. Usiwe mtu usiyejali, ambaye upo tayari kwa lolote, hata kama ni kuachana na mwenzi wako. Hii ni kati ya sumu hatari zitakazokufanya uishie kuachika kila siku.
Bado kuna mengi ya kujifunza marafiki zangu. Wiki ijayo tutaendelea. USIKOSE!
Joseph Shaluwa ni Mshauri wa Mambo ya Mapenzi, anayeandikia magazeti ya Global Publishers. Ameandika Vitabu vya True Love, Let’s Talk About Love na Who is Your Valentine? vilivyopo mitaani.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Jessica Ngowi Is Sheria Ngowi’s New Womenswear Creative Director.


Sheria Ngowi today announced that it has appointed Jessica Ngowi as its new Womenswear creative director.


TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

HEW HIT:Tonight - J-Ryder Feat. Dar City Boyz (DCB)


 click here to download
 http://snd.sc/LcE23a


It's that summertime, everything is good. What follows is a collaboration
from two different places. A Club Joint, for party people and all fans who
enjoy great music. The Song is called *Tonight* and *J-Ryder *joined with *Dar
City Boyz (DCB)* which comprises of *Big Flow Santanna*, *Imma*, and *Lil
Harsh* to complete the song. We greatly appreciate and thank all for your
support on this song. We have a great feeling it's going to reach far and
also taking the Tanzanian Music to the next level.
Producer : *J-Ryder*
Vocals : Dar City Boyz (DCB), Recorded at *Marshalz Studios (India)*
Links
http://twitter.com/#!/TEAMDARCITYBOYS
J-Ryder - http://www.facebook.com/pages/J-Ryder/152161138135913
Immo - http://www.facebook.com/emmanuel.mlowe
Big Flow Santanna - http://www.facebook.com/profile.php?id=1811878087
Lil Harsh - http://www.facebook.com/hashim.miraji
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

MTITU AFICHUA SIRI YA MBWA WA UWOYA, RAY

Mbwa wa Irene Uwoya.
Na Erick Evarist
MWIGIZAJI wa ‘long time’ Bongo, William Mtitu ameweka bayana kuwa hakupenda aina ya mbwa aliokuwa akiwamiliki ndiyo maana aliamua kumuuzia Irene Uwoya.
Akichezesha taya na Ijumaa kwenye ofisi zake zilizopo Magomeni jijini Dar, Mtitu alisema alifikia uamuzi wa kuwauza mbwa hao baada ya kubaini hawawezi kazi ya ulinzi.
“Mi’ nilishawishiwa na rafiki yangu kuwanunua nikidhani ni mbwa wa ulinzi nyumbani kumbe ni mbwa koko.
“Sasa Mbwa gani kila unapotaka kwenda na yeye anakufuata, siyo mkali wala nini ndiyo akatokea Uwoya nikamuuzia, nasikia na yeye kamuuza mmoja kwa Ray,” alisema Mtitu.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

UNAWEZA KUMPENDA KABLA HUJAMUONA?

HAPA ndiyo sehemu pekee ya kupanua mawazo na kukuza ubongo wako juu ya mambo yanayohusu uhusiano na mapenzi. Kama ni mara yako ya kwanza kuanza kupitia ukurasa huu, umekutana na kona muhimu sana. Huna cha kupoteza. Utajengeka kila siku.
Rafiki zangu, leo nimekuja na mada mpya baada ya kuhitimisha ile ya wiki iliyopita. Nina imani kuna mengi mliyojifunza. Mada ya leo inatokana na maswali mengi ya aina moja niliyoyapata kwa muda mrefu kutoka kwa wasomaji mbalimbali.
Hebu msikie huyu: “Pole na kazi kaka Shaluwa, kuna kaka nawasiliana naye. Kiukweli tumezoeana sana, juzi hapa amesema eti ananipenda na anataka kunioa. Mimi nipo Mbeya, yeye anaishi Dar es Salaam.
“Hatujawahi kuonana, zaidi ya kuzungumza kwa njia ya simu tu. Nilifahamiana naye baada ya kukosea namba, ndipo tukakubaliana kuwa marafiki. Tafadhali naomba msaada wako maana ninachanganyikiwa kabisa. Ni kweli ananipenda?”. 
Kilio kama hicho nilikipata pia kutoka kwa msomaji mmoja ambaye naye sitachapa jina lake gazetini. Huyu alisema: “Nimekutana na rafiki kwenye Facebook, tunawasiliana mara kwa mara, ninahisi kumpenda huyo msichana. Naye ana kila dalili za kunipenda, tatizo sijaanza tu kumweleza. Hivi, inawezekana kweli tukapendana kabla ya kuonana?”
Bila shaka kuna picha umeipata kupitia maswali ya wasomaji hao wawili. Niliwaahidi kuandika mada gazetini ambapo ndipo wangepata majibu yao. Je, wewe upo kwenye kundi gani?
Umewahi kukutana na jambo hilo? Unadhani unaweza kumpenda mtu kabla ya kukutana naye? Sauti pekee inaweza kumfanya mtu ampende mwenzake kwa dhati na mapenzi yao yakadumu? Twende tukajifunze.

INAWEZEKANA?
Hili ni jambo la kwanza linalotakiwa kupatiwa majibu kabla ya kuendelea na mada hii. Huu ni mtazamo hasi. Jibu kwa kifupi tu ni haiwezekani. Utawezaje kumpenda mtu ambaye hujamuona?
Misingi ya kumpenda mwingine ikoje? Kanuni zipo wazi; KUPENDA ndiyo jambo la kwanza, ambapo ukweli ni kwamba huanza na kutamani, sasa itawezekanaje kumtamani mtu ambaye hujawahi kukutana naye?
Baada ya kupenda, kuna mambo mengine ya msingi ambayo ni muhimu kuzingatiwa ili kujihakikishia kwamba uliyempata ni mwenzi sahihi. Kuna suala la kuchunguzana tabia n.k, yote haya yatawezekana vipi kufanyika kabla ya kukutana?
Najua ni wengi wamekumbana na hili ninalolizungumzia hapa, unashindwa cha kufanya na kubaki gizani. Leo utarudi kwenye mwanga! Unajua chanzo cha yote hayo ni nini? Twende kwenye kipengele kinachofuata.

HUANZA HIVI...
Chanzo kikuu cha udanganyifu huu wa mapenzi huwa ni vyombo vya mawasiliano. Mfano mtu amepiga simu amekosea namba...mara anaanza ‘uko wapi? Haina neno, tunaweza kuwa marafiki?’
Mazoea yakizidi, kila mmoja huanza kumwuliza mwenzake vitu anavyopendelea na mambo mengine. Baadaye wanatongozana! Huelezana mambo mengi sana na ahadi nyingi wakiamini kwamba wanapendana kwa dhati!

MAPENZI YA HISIA
Kimsingi sababu ya haya yote ni hisia tu. Njia ya mawasiliano inaweza kukoleza au kuimarisha uhusiano ambao tayari upo. Mfano kama unaishi Moshi na mpenzi wako yupo Mwanza, mnaweza kuboresha uhusiano wenu kwa kuwasiliana kwa njia ya simu, waraka pepe na mitandao ya kijamii.
Kinachotokea kwa marafiki wapya ambao wanahisi tayari ni wapenzi na wanapendana ni zile hisia za ndani zinazowaingia wakati wa mawasiliano yao. Pengine walianza kuzungumzia mambo ya mapenzi na kujikuta wakitamani kuwa karibu.
Jambo kubwa zaidi ni kwamba mhusika hutawaliwa zaidi na hisia, maana kwa sababu hawafahamiani, watakuwa wanauliza; ‘Wewe ukoje? Mrefu, mfupi, mwembamba, mnene au?’ halafu mwenzake atamjibu, ‘mrefu kiasi, si mnene sana, kifupi nina umbo namba nane...navutia na ni maji ya kunde’. 
Kifupi mtu anaweza kujielezea vyovyote atakavyo, hivyo kumfanya mwenzake amtengeneze ajuavyo kichwani mwake na kujihakikishia kwamba anampenda kwa dhati mwenzake kumbe anajidanganya!

TABIA BANDIA
Mbaya zaidi ni kwamba, wakati wapenzi hawa wanaojidanganya wakiendelea kuwasiliana si rahisi kujuana vizuri kitabia kwa sababu wengi huonesha tabia bandia. Mambo yao ya ndani wanayaficha kwa nguvu na kuonesha mema tu.
Hapo ndipo mwanzo wa penzi feki kwa kudanganyika na tabia za kutengeneza.

HULKA MBAYA
Kuna wengine ni tabia zao za asili. Amezoea kupata wapenzi kwa kupitia kwenye simu na mitandao ya kijamii. Usishangae kuna wengine wanapiga namba hata wasizozijua, akikutana na mtu wa jinsia tofauti na yake, anaanza mambo yake. Akimaliza haja zake anakuacha!

ACHA KUJIDANGANYA
Ni vizuri sasa ukatoka kwenye ulimwengu wa giza na kurudi kwenye ulimwengu unaonekana. Kwa hakika ni vigumu sana kumpenda mtu ambaye hujamuona, labda kama unataka kucheza na muda wako.
Wako anakuja, vuta subira ukifanya mambo yako kwa usahihi. Usijidanganye na matapeli wa mapenzi. Wapo ambao wanafanikiwa kuingia kwenye mapenzi lakini mwisho wao hauwi wenye mafanikio.
Penzi la dhati hubebwa na vitu vingi sana, ukiachana na UPENDO kuna suala la tabia na mengine mengi ambayo huwezi kuyajua kwa njia ya kuwasiliana pekee. Utajihakikisha umempenda kwa kumtengeneza kichwani mwako, mwisho wa siku unakutana na mtu ambaye yupo tofauti na mawazo yako, itakuwaje hapo?
Joseph Shaluwa ni Mshauri wa Mambo ya Mapenzi anayeandikia magazeti ya Global Publishers. Ameandika vitabu vya True Love, Let’s Talk About Love na Who is your Valentine? vilivyopo mitaani.
KWA HABARI ZAIDI ZA MAHUSIANO NA NYINGINE INGIA:
                    
                                GLOBAL PUBLISHERS
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Makahaba na michezo ya Olimpiki London

London 2012: Je michezo ya Olimpiki italeta makahaba zaidi?

Kabla ya kuanza kwa msimu wa michezo ya kimataifa mfano kombe la dunia na michezo ya Olimpiki kwa kawaida, kitu ambacho huanza utakisikia kwanza na zaidi ni hofu ya ongezeko la biashara ya ukahaba pamoja na tahadhari ya biashara haramu ya ngono. Hofu hii inatokea kwa sababu ya ongezeko la watu. Lakini je, biashara ya ukahaba itaongezeka kweli kwa sababu ya michezo ya olimpiki 2012?

Inaonekana kama kila wakati shindano la kombe la dunia au michezo ya olimpiki inapokaribia, bila shaka ndipo tahadhari kutoka kwa vyombo vya habari vya kimataifa, mawaziri wa serikali na hata polisi nazo zinapoongezeka.

Wote huelezea hofu kuwa maelfu ya wanawake watauzwa katika biashara ya ukahaba hadi katika taifa mwenyeji ili kukidhi mahitaji ya kingono ya makundi ya watu wanaowasili nchini humo.

Ujumbe sawa na huo umekuwa ukitolewa kuhusiana na michezo ya Olimpiki 2012 mjini London.

Mwezi Januari mwaka 2010, aliyekuwa waziri wa michezo ya Olimpiki katika serikali iliyopita, Tessa Jowell, aliambia wabunge kuwa "michezo ya kimataifa wakati mwingine inaweza kufanya biashara ya ngono kukithiri na jambo hili halikubaliki. Nitajitolea kuhakikisha kuwa wanaoendesha biashara hizo hawatumii michezo ya London kwa manufaa yao."

Dennis Hof, anayemiliki jumba kubwa sana la makahaba la Moonlite Bunny Ranch, lililoko mjini Nevada, Marekani, anasema kuwa London ijiandae kwa wasichana 1,000 wataoletwa nchini humo kwa sababu ya biashara za ngono kutoka kusini mwa kanda ya Asia Mashariki, Albania na barani Afrika. Wote wataletwa na makundi yanayohusika na uhalifu pamoja na biashara ya mihadarati.

Makahaba

Hof, anayetaka aruhusiwe kuendesha jumba halali la biashara ya ngono mjini London wakati wa michezo hiyo, anasema kuwa utabiri wake umejikita katika kile alichokiona wakati wa michezo ya olimpiki ya mwaka 2010 mjini Vancouver, Canada.

Je onyo hizi zina uhakiki?

Michezo ya Olimpiki, mwaka 2004 mjini Athens, ndio ilionekana kuwa michezo ya kwanza ya kimataifa kuzua hisia hizi baada ya kuelezewa hofu juu ya ongezeko la makahaba. Mji huo ulielezea kuona ongezeko maradufu la biashara ya ngono.

Hata hivyo ripoti ya shirika la kimataifa dhidi ya biashara haramu na ulanguzi wa wanawake, (GAATW), inaonyesha kuwa idadi ya visa hivyo mjini Athens mwaka 2004 iliongezeka hadi watu 181, kutoka kwa 93 mwaka 2003.

Kabla ya kuanza kwa dimba la kombe la dunia nchini Ujerumani mwaka 2006, onyo kama hizi zilitolewa na vyombo vya habari na maafisa wengine wakuu lakini kulingana na ripoti iliyotolewa na Muungano wa Ulaya kuanzia Januari mwaka 2007, serikali ya Ujerumani ilipata tu visa vitano vya ukahaba vilivyohusishwa na dimba hilo.

Ripoti hiyo ilisema kuwa ongezeko la biashara haramu ya ngono pamoja na ulanguzi wa watu kwa sababu ya kutumiwa kwa faida za kingono, wakati wa kombe la dunia mwaka 2006 nchini Ujerumani haikutokea kama ilivyokuwa imehofiwa. Na kwamba madai ya makahaba 40,000 kuingia nchini humo hayakuwa ya kweli kama ilivyoripotiwa na vyombo vya habari.

Ili hali kombe la dunia la mwaka 2006, limetumiwa kama mfano wa kuonyesha namna ambavyo idadi kubwa ya makahaba walilipwa na idadi kubwa ya watu waliohudhuria dimba hilo kwa mahitaji yao ya kingono.

Tukisalia katika kombe la dunia, utafiti uliofadhiliwa na shirika la umoja wa mataifa la kukadiria idadi ya watu, UNFP, iliyofanywa nchini Afrika Kusini wakati wa kombe la dunia mwaka 2010, iligunduliwa kuwa hapakuwa na tofauti kubwa katika ongezeko la wanaume waliotafuta huduma za makahaba wakati wa mchuano huo.

Majumba ya makahaba kwa picha

Lakini kulikuwa na wasiwasi kuwa kati ya makahaba 40,000 na 100,000 kutoka kote duniani wangeingia nchini humo kwa sababu ya shindano hilo.

Utafiti huo unasema kuwa licha ya taarifa za vyombo vya habari kabla ya michezo hiyo , hapakuwa na ukweli wa kuongezeka kwa biashara ya ngono na kuongezeka kwa makahaba kama ilivyokuwa imetabiriwa.

Wengi sasa wanatumia mifano ya michezo ya olimpiki iliyofanyika nchini Ugiriki, Ujerumani na Afrika Kusini kusema kuwa London bora ijitayarishe kwa ongezeko la makahaba.

Tayari kundi moja linalowakilisha makahaba mjini London, x:talk, lmetoa wito kwa polisi kukoma kuwakamata, kuwazuia au kuwarejesha makwao watakaokamatwa hadi michezo hiyo ya Olimpiki iishe.

Msemaji wa kundi hilo ansema kuwa pia msako wa polisi dhidi ya maumba ya makahaba hasa mashariki mwa London inasbabisha makahaba kutorokea kwingineko kutoka kwa mashirika yanayowasaidia makahaba hao na hata vituo vya afya , na hivyo kusababisha wito wa kuwataka polisi kukoma kuwakamata makahaba.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

TAWI LA CHADEMA WASHINGTON DC LAZIDI KUKUSANYA WANACHAMA

Mwenyeketi wa Tawi la Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Washington DC, Mhe. Kalley Pandukizi, pamoja na katibu wake, Mhe. Libe Mwang'ombe wakipata picha ya pamoja na Linda Bezuidenhout Atlanta, Georgia na wanachama wa tawi la Chadema Washington DC.

---
Katika miaka ya nyuma Linda aliwahi kusponsor matukio mbalimbali kwenye miaka ya 1990 wengi wao wakimjua kwa Linda Express nchini Tanzania ambaye hivi sasa anajishughulisha na biashara ya nguo za kiume milanovita.com pamoja na za kike ambazo anadesign mwenyewe kwa brand name ya Linda kutoka Atlanta, Georgia nchini Marekani.


TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

HAWA NDO MAFREEMASON WALOTINGA CLOUDS FM......ahahahah

Pichani ni Dkt. Kemu Mzee (kushoto) na Alhaj Prof. Dkt. Salim Kungulila (kulia) wanaojiita Freemasons walio temebele kituo cha Clouds FM leo asubuhi kwenye kipindi cha Leo tena na kuelezea ufreemason wao

Wanadai wao wanafundisha dini zote na kudai kua kila mtu duniani ni Freemason na pia wafafanua maana halisi ya ufreemasons ila mwisho wasiku walishindwa kujibu kama wao ni mafreemasons au laaah! Wakaishia kusema wao ni WaashiHuru…

Walipo ulizwa kama freemason wanaabudu shetani wakashindwa kujibu.

Dkt. Kemu Mzee alisema ufreemason ni kitu ambacho hukioni na ni kama kuuza bidahaa haraka haraka kabla ya mwenzio so hapo wewe uliye uza haraka haraka ndo unatajirika haraka.

Walipo ulizwa juu ya masharti ya kujiunga waksema yanapatikana ofisini kwao na ni lazima mtu apate matibabu yao ambayo ni lazima na kuongezea ni sawa na kujiunga na chama fulani ukafuata masharti yao so kwa upande wao tiba yao ndo lazima.

Na Alhaj Prof. Dkt. Salim alisema watu wanapo ambiwa majini wanaogopa lakini watu wasihofu maana majini ni kama mashine. Mpaka sasa sielewi alimaanisha nini hahaha!!!

Kwa kumalizia waliulizwa kama freemason wanatakiwa kutoa sacrifice (kafara) ya ndugu wa karibu wakasema sacrifice (kafara) kila mtu anatoa wakristo au waislamu. Hiyo yakutoa watu ni uzushi pengine.

Hahaha hakuna siku nimecheka kama leo maana hawa jamaa nahisi walienda kuuza sura walikuwa wanapiga chenga maswali na kujibu yao tu.

Kwa hiyo kuconclude na kutokana na maelezo yao wao wamejiita WAASHIHURU tafsiri yake FREEMASON!
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

FAHAMU JINSI YA KULINDA ACCOUNT YAKO MTU ASIWEZE KUHACK!!!

After LinkedIn: How to protect your password from hacks


The constant battle for Internet security saw another brazen attack this week as Russian hackers published millions of passwords they collected after hacking the professional-networking site LinkedIn.

Then, hours later, dating site eHarmony announced that a "small fraction" of its users -- others were saying 1.5 million -- were compromised by a similar attack. Security professionals suspect the same hackers may have done it.

"That's what we think," said Graham Cluley, a senior technology consultant with Sophos Security. "It was shared in the same places. The content is very similar. And the timing. All of these factors just make it seem like too much to be a coincidence."

It's enough to make some Web users throw up their hands. If the sites we use on a daily basis can't keep our password data secure, how are we supposed to keep ourselves safe?

But security experts say there are still plenty of steps we can take (even if too many people aren't following them).

How to check if your password was stolen

Password-management firm LastPass has released a secure tool to see if your password was among the more than 6 million stolen from LinkedIn. LastPass created a similar tool for people worried about the security of their eHarmony accounts.

Your password still matters

Even in cases such as the LinkedIn breach, when it's a website, not a personal account, that's being hacked, the strength of your password can still help keep you safe.

On sites such as LinkedIn, stored passwords are "hashed," meaning the site uses an algorithm to encode them. So, even if hackers get the data, they still have to unravel them before they're useful.

"Don't give up. Don't think this is all futile," Cluley said. "Choose a long, hard-to-crack, unique password. Not dictionary words. Not a sequence of numbers -- use something that basically looks like gobbledygook. Those will be tougher for the bad guys to crack."

In the case of LinkedIn, there are reports that as many as 60% of the encrypted passwords stolen have been decoded, raising questions about the strength of its security system.

Be careful of post-hack e-mails

When there's a well-publicized security incident on a well-known website, online crooks are more than happy to pile on.

In the wake of the LinkedIn hack, security professionals were already reporting incidents of users receiving "phishing" attempts -- e-mails that look like official communications from LinkedIn. Instead, these messages try to get users to reveal personal data that identity thieves could be use. Or they include links that, when clicked on, can install malware on an unsuspecting user's computer.

"We are investigating the exact details but in the meantime please DO NOT CLICK on links in email to change or verify account information, at LinkedIn.com or on any other membership site," Cameron Camp of ESET Smart Security wrote on the company's blog. "Instead, navigate to the site directly by typing in the address bar in your browser."

Use different passwords for different sites

Cluley notes that the hackers who attacked LinkedIn and eHarmony may not have even been interested in information from those sites.

In many cases, they'll be trying to use the passwords they find on other sites and accounts. Many banks require additional information to log in. But accounts such as Amazon, eBay and PayPal, for example, could be compromised if the user has one password across multiple sites.

"If you get hacked in one place, you get hacked everywhere," he said.

Lots of folks complain about how hard it is to remember multiple passwords. But there are free online tools that will store and use them for you. Cluley mentioned several, including KeePass, 1password and LastPass.

Cluley recommends those tools over letting your Web browser store passwords for you, because there have been cases of security flaws in some browsers, which hackers have exploited to access user data.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Thursday, June 7, 2012

LULU KABADILIKA JAMANI....


MAZINGIRA ndani ya Gereza la Segerea jijini Dar yamemlazisha msanii wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ kubadili tabia bila ya kupenda, Amani linakuhabarisha.
Lulu ambaye ni mshukiwa namba moja katika kifo cha msanii wa filamu nchini, Steven Kanumba, hivi sasa analazimika kuvaa nguo ndefu na kutinga hijabu tofauti na alivyokuwa uraiani.
Kwa mujibu wa kumbukumbu zilizopo katika makabrasha yetu, msanii huyo kabla ya kukumbwa na tuhuma hizo, akiwa uraiani aliwahi kufanya mahojiano na waandishi wa Global Publishers na kudai kuwa hawezi kuvaa nguo ndefu kwa kuwa zinamuwasha mwilini.
Hata hivyo, imebainika kuwa hayo yalikuwa ni maneno ya rejareja ya Lulu kwa lengo la kujitetea kwa mapaparazi.
Haya yote yamekuja kufuatia msomaji mmoja kupiga simu ofisi za Global akihoji kuhusu habari ya staa huyo kudai nguo ndefu zinamuwasha.
“Jamani mimi naitwa mama Diana, naishi huku Tabata. Kuna wakati mliandika madai ya Lulu kwamba anasema akivaa nguo ndefu anawashwa mwilini, siku hizi kila nikiangalia picha zake za mahakamani namwona amevaa nguo ndefu. Je, hawashwi?
“Nauliza kwa sababu hivi karibuni mliandika Lulu apata gonjwa baya gerezani, nikafikiri lilitokana na kuwashwa,” alisema msomaji huyo.
Hata hivyo, alifahamishwa kuwa ugonjwa uliompata msanii huyo gerezani hautokani na kuvaa nguo ndefu.
“Kwa sasa Lulu anatinga nguo ndefu za kila aina na wala halalamiki kuwashwa,” paparazi wetu alimjibu mwanamke huyo.
Kesi inayomkabili msanii huyo itaendelea tena katika Mahakama Kuu Juni 11, mwaka huu na anatarajiwa kutinga akiwa na nguo ndefu nyingine.


TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

DAR INATISHA


JIJI la Dar es Salaam na viunga vyake hasa maeneo ya maegesho ya magari (parking), viwanja vya wazi na ufukweni, linatisha kwa vitendo vya ngono za rejareja vikiongozwa na watu maarufu, Amani limefanya uchunguzi wake na hii ndiyo ripoti kamili.
Kwa nyakati tofauti, hivi karibuni, gazeti hili lilinasa matukio yenye kutia kinyaa yakifanywa waziwazi na wakati mwingine mchana kweupe.
Katika maeneo tofauti, kamera yetu iliwanasa mabinti wadogo ‘wakidendeka’ hadharani bila kujali umati uliowazunguka.

MAENEO HATARINI
Maeneo yanayotajwa kukithiri kwa uchafu huo jijini Dar ni pamoja kwenye mikusanyiko ya wazi kama Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni Makaburini, Buguruni, Ufukwe wa Coco na kwenye ‘parking’ mbalimbali za kumbi za starehe.

NDANI YA LEADERS
Mabinti waliotambuliwa kwa jina mojamoja, Husna na Vai walinaswa kwenye Viwanja vya Leaders Club wakifanya matendo machafu ya kisagaji.





MLIMANI CITY
Jumapili moja, Amani likiwa ‘rovingi’ liliwamulika ‘masistaduu’ ambao walitajwa kwa jina mojamoja, Jack na Teddy kwenye ‘parking’ za Mlimani City ambao wanadaiwa kuwa miongoni mwa kundi la wadada wanaoligeuza Jiji la Dar kuwa kama Sodoma na Gomora kwa kujihusisha na vitendo vichafu vya ngono.

COCO BEACH
Pia ‘patroo’ yetu ilimtia kibindoni mwigizaji wa muvi za Kibongo, Isabela Francis ‘Vai wa Ukweli’ ‘akidendeka’ na mwanaume aliyedaiwa kuwa ni ‘kuku mtamu’ kwenye Ufukwe wa Coco.

MANGO GARDEN
Kwenye Ukumbi wa Mango Garden, demu aliyetajwa kwa jina moja la Jack naye aliingia mtegoni baada ya kunaswa akiwalegezea zipu wanaume bila kujali macho ya kadamnasi.

FUKWE ZA BAGAMOYO
Mbali na maeneo hayo, pia fukwe nyingi zinazoanzia Dar hadi Bagamoyo nazo zilifumuliwa na ‘shushushu’ wetu aliyeshudia uchafu wa ajabu wa ngono rejareja zikihusisha dada zetu na watasha.




WAZAZI
Dawati la Amani linatumia fursa hii kuwataka wazazi kuwatupia macho watoto wao hasa mabinti kwani hali ni mbaya na watachuma majanga muda si mrefu.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

MAKALIO MAPYA YA KICHINA YATUA RASMI BONGO

KUFUATIA taarifa kuwa, dawa za Kichina za kuongeza makalio zina madhara kwa watumiaji, njia mbadala ya kukuza maeneo hayo nyeti imegunduliwa na imeanza kutumika kwa kasi Bongo, Amani linakuhabarisha.
Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wetu umebaini kuwa njia hiyo inayotumiwa kwa sasa na wanawake wengi hasa wa mjini si ya kumeza wala kupaka dawa bali ni ya kuvaa taiti zilizojaladiwa vifaa maalum vilivyotuna mithili ya makalio.

Jinsi inavyokuwa
Akizungumza na Amani, mmoja wa wafanyabiashara wa ‘makalio’ hayo aliyejitambulisha kwa jina la Mama Sanura, alisema ubunifu huo umekuja kufuatia utafiti kuonesha kuwa baadhi ya wanawake wanatamani kuwa na makalio makubwa ila wanaogopa kutumia dawa za Kichina.
“Wanawake wengi wanatamani kuwa na makalio makubwa ili wawadatishe wanaume lakini hawakujaaliwa kuwa nayo, wapo ambao wamefikia hatua ya kutumia zile dawa za Kichina na ilipobainika zina madhara wameacha.
“Watu wakakaa na kuumiza vichwa, ndipo walipogundua njia hii ambayo ni salama kwani anachotakiwa kufanya mwanamke ni kununua taiti hizo ambazo ndani yake kuna kina kitu chenye shepu ya kalio na hips, akivaa na suruali au sketi, huonekana amejaaliwa kumbe hamna kitu,” alisema mama huyo mwenye duka lake la nguo maeneo ya Kariakoo, Dar.

Wateja ni nani?
Imeelezwa kuwa wanaonunua vifaa hivyo ni wanawake wakiwemo pia baadhi ya wanaume ambao huwanunulia wapenzi au wake zao ili kuwafanya wawe na muonekano tofauti.
“Huwezi kuamini si wanawake tu wanaokuja kununua vifaa hivi, wapo pia baadhi ya wanaume ambao huwanunulia wapenzi wao na kati ya hao wamo pia mastaa. Ndiyo maana kuna ambao unawaona leo ana kijungu, kesho hana,” alisema mama huyo.

Lengo la kufanya hivyo ni lipi?
Uchunguzi umebaini kuwa baadhi ya wanawake hutumia makalio hayo ili kuwadatisha wanaume wanapokatisha mitaani na wengine ili kuwarusha roho wanawake wenzao.
“Kuna wanawake wana tabia za ajabu sana, kwa wengine kuwa na kalio ni sifa kwao na ndiyo maana baadhi yao huvaa wanapokwenda kwenye sherehe au ‘outings’ za kawaida ili tu kuwarusha roho wenzao.
“Lakini wapo pia wanawake wanaoyatumia ‘makalio’ hayo kutafuta soko kwani hawa wanaojiuza wameshajua baadhi ya wanaume ni wabovu sana kwa wanawake wenye makalio,” anasema mama Sanura.

Wadau wanasemaje?
Kila mmoja anaweza kuwa na maoni yake kuhusiana na matumizi ya makalio haya mapya ya Kichina lakini wengi walioongea na Amani wamekuwa wakiponda wale wanaovaa taiti hizo wakidai ni ulimbukeni.
“Huu ni ulimbukeni jamani, kama wewe hukujaaliwa kuwa na kalio orijino, hilo feki litakusaidia nini? Kama unavaa ili kuwadatisha wanaume, je ukiwa naye chumbani atanufaika na nini?
“Ifike wakati tukubaliane na maumbile tuliyojaaliwa na Mungu, kuvaa taiti hizo ni kujichoresha tu kwani leo unaonekana una wowowo kisha kesho utaonekana wa kawaida,” alisema Elizabeth wa Kinondoni, Dar es Salaam.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

KUAMBIANA MIKONONI MWA POLISI

MWIGIZAJI mwenye rekodi ya kutupwa selo mara kwa mara, Adam Kuambiana (pichani), safari hii amekamatwa na polisi kwa madai ya kumshushia kipigo mfanyabiashara, Fadhili Joseph.
Chanzo kilisema, Juni 3, mwaka huu Kuambiana alikunywa bia kwenye baa ya Fadhili, Sinza Mori, Dar na kushindwa kulipa, hivyo kulazimika kuacha ‘laptop’ yake ili aikomboe atakapolipa deni hilo.
“Tofauti na makubaliano, siku ya pili msanii huyo alimfuata Fadhili na kumtaka ampe laptop yake kwa nguvu bila kulipa deni hilo, alipokataa, alimshushia kipigo Fadhili mpaka alipopata msaada wa polisi,” kilieleza chanzo hicho.
Mapaparazi wetu walifika Kituo cha Polisi Kawe ambapo walikuta mlalamikaji amefungua jalada la kesi lenye namba KW/RB/5761/2012 SHAMBULIO. Kesi hiyo imehamishiwa Kituo cha Polisi Kijitonyama ‘Mabatini’ kwa vile ndiyo kituo cha karibu na eneo la tukio.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

CHAZ BABA ATAKA PENZI KWA NGUVU

PREZIDAA wa Bendi ya Mashujaa, Charles Gabriel ‘Chaz Baba’ juzikati aliwashangaza watu kufuatia kumng’ang’ania mwigizaji wa sinema za Kibongo, Zamda Salim ‘Zam Minaj’ ili aondoke naye kuelekea kwake.
Tukio hilo la kutaka kwenda kupewa penzi la lazima, lilichukua nafasi ndani ya Ukumbi wa New Maisha Club, Dar usiku wa kuamkia Mei 29, mwaka huu.
Mwanamuziki huyo alimfuata Zamda na kumwambia kwamba siku nyingi amekuwa akimtongoza na kumpa ahadi hewa kwa hiyo siku hiyo ilikuwa arobaini yake.
“Leo sikubaliani na ‘sound’ zako, lazima tuondoke wote, tena sasa hivi,” alisikika akisema Chaz huku akimvuta demu huyo.
Hata hivyo, Zamda aliweza kuponyoka kutoka mikononi mwa Chaz na kutokomea kusikojulikana.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

KILA LA KHERI DADA SHY-ROSE BHANJI

      



                             Now ni mbunge kamili wa Bunge la Africa Mashariki hapo akila kiapo


Shy-Rose Bhanji akisaini nyaraka za kiapo.


KILA LA KHERI DUA NJEMA NAKUOMBEA UKAWE MFANO WA KUIGWA NA WENGI NA MUNGU AZIDI KUKUBARIKI NA KUFANIKISHA KILA JEMA UPANGALO KWA AJILI YA TANZANIA NA WATANZANIA.



TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Wednesday, June 6, 2012

TAARIFA KUHUSU MECHI YA TAIFA STARS NA GAMBIA


Release No. 086
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Juni 6, 2012
KIINGILIO MECHI YA TAIFA STARS, GAMBIA 3,000/-
Kiingilio cha chini ya mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Gambia (The Scorpions) itakayochezwa Jumapili (Juni 10 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni sh. 3,000.
Watazamaji watakaolipa kiingilio hicho ni watakaokaa kwenye viti vya rangi ya bluu na kijani ambavyo ni 36,693 kati ya jumla ya viti 57,558 vilivyopo katika uwanja huo wa kisasa. Kiingilio kwa viti vya rangi ya chungwa ni sh. 5,000.
Kwa upande wa VIP C watalipa sh. 10,000 wakati VIP B ni sh. 20,000. Kiingilio kwa jukwaa la VIP A ambalo linachukua watazamaji 748 tu ni sh. 30,000 kwa mechi hiyo itakayoanza saa 10 kamili jioni.
Tiketi zitaanza kuuzwa Jumamosi (Juni 9 mwaka huu) kuanzia saa 2 asubuhi kwenye vituo vya Mgahawa wa Steers ulioko Mtaa wa Ohio na Samora, Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Soko Kuu la Kariakoo na Uwanja wa Taifa. Siku ya mechi pia mauzo yatafanyika katika vituo hivyo na baadaye kuhamia Uwanja wa Taifa.

GAMBIA YATARAJIA KUINGIA LEO DAR ES SALAAM
Timu ya Taifa ya Gambia (The Scorpions) inatarajia kuwasili nchini wakati wowote kuanzia leo (Juni 6 mwaka huu) tayari kwa ajili ya mechi dhidi ya Taifa Stars.
Kamati ya Maridhiano inayoendesha Chama cha Soka Gambia (GFA) hadi leo mchana ilikuwa haijatuma taarifa rasmi kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) juu ya ujio wake.
Lakini vyombo vya habari vya Gambia vimeripoti kuwa timu hiyo ikiwa na wachezaji 23 na viongozi tisa ilitarajiwa kuondoka huko leo kuja Dar es Salaam tayari kwa ajili ya mechi hiyo inayosubiriwa kwa hamu na washabiki wengi nchini.
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa GFA aliyekaririwa na vyombo vya habari vya nchi hiyo, Bakary Balder, msafara wa timu hiyo utaongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Vijana na Michezo, Malang Jassey.
Mbali ya Jassey, viongozi wengine katika msafara huo ni Ofisa Utawala wa timu Modou Sowe, Kocha Luciano Machini, makocha wasaidizi Peter Bonu Johnson na Lamin Sambou, Kocha wa makipa Alhagie Marong, mtaalamu wa tiba mbadala (physiotherapist) Pa Matarr Ndow, Mtunza vifaa Sanna Bojang na Daktari wa timu Kalifa Manneh.
Wachezaji ni Musa Camara, Abdou Jammeh, Momodou Futty Danso, Lamin Basmen Samateh, Ousman Koli, Pa Saikou Kujabi, Mustapha Kebba Jarju, Yankuba Mal Ceesay, Demba Savage, Saihou Gassama, Alieu Darboe, Momodou Ceesay, Pa Modou Jagne, Tijan Jaiteh, Bubacarr Sanyang, Christopher Allen, Musa Yaffa, Sulayman Marr, Mamut Saine, Hamsa Barry, Ali Sowe, Omar Colley na Saloum Faal.
PROGRAMU YA TAIFA STARS KWA MECHI YA GAMBIA

JUMATANO JUNI 6
01.00 asubuhi Mazoezi- Uwanja wa Karume
10.00 jioni Mazoezi- Uwanja wa Taifa

ALHAMISI JUNI 7
10.00 jioni Mazoezi- Uwanja wa Taifa

IJUMAA JUNI 8
10.00 jioni Mazoezi- Uwanja wa Taifa

JUMAMOSI JUNI 9
04.00 asubuhi Mkutano na Waandishi wa Habari- Ukumbi wa TFF
11.00 jioni Mazoezi- Uwanja wa Taifa

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Marekani yathibitisha kuua al-Libi



Ikulu ya White House imesema kwamba imekabili kundi la kigaidi la Al Qaida pigo kubwa kwa kumwua naibu wa mkuu wa kundi hilo, Abu Yahya al-Libi, nchini Pakistan.

Maafisa wa Marekani wamesema kuwa alilengwa katika shambulio lilolofanywa na ndege isiyo na rubani ya Marekani katika maeneo ya mashambani ya Pakistan mnamo Jumatatu.

Ikulu ya White Housae ilithibitisha kuwa hii ni mara ya pili chini ya muda wa mwaka mmoja ambapo Marekani imemwua kiongozi mkuu wa Al-Qaida, hatua ambayo inakaribia kuangamiza kundi hilo la kigaidi.

Afisa wa cheo cha juu katika serikali ya Marekani, amethibitishia BBC kuwa shambulio la ndege isiyo na rubani lililofanywa katika maeneo ya mashambani lilimlenga Abu Yahya al-Libi, ambaye alidaiwa kupanda cheo na kushikilia nafasi ya pili katika kundi hilo kufuatia kifo cha Osama Bin Laden, mwaka jana.
Obama athibisha kuawa kwa al-Libi

Serikali ya Rais Obama imethibitisha kuwa Abu Yahya al-Libi ni mmoja wa wale waliouwa katika shambulio hilo la ndege isiyo na rubani.
Osama Bin Laden

Osama Bin Laden aliyeuawa mwezi Mei mwaka uliopita

Wadokezi wa Serikali ya Marekani walisema kuwa kiongozi huyo wa Al-Qaida alikuwa alikuwa lengo la shambulio hilo la eneo linalodhaniwa kuwa maficho ya wapiganaji kadhaa wa Al Qaida Kaskazini mwa Wazirstan karibu na mpaka wa Afghanistan.

Marekani ilimtaja Al Libi kama anayeshikilia cheo cha pili katika kundi hilo, anayesimamia shughuli za kila siku katika eneo hilo la mashambani na maeneo mengine yaliyo na uhusiano mkubwa na kundi hilo. Afisa mmoja wa Marekani alisema kifo cha kiongozi huyo wa Al Qaida ni pigo kubwa kwa kitovu cha Al Qaida.

Ingawa Marekani imeshangilia kuuawa kwa viongozi hao wa Al Qaida na wapiganaji wa Taliban kila mara wanapotumia ndege hiyo isiyo na rubani; uhusiano wa Marekani na Pakistan umeendelea kuzorota kwa sababu ya mashambulizi hayo.

Katika mashambulizi mengine raia wamewahi kufariki kimakosa katika Pakistan na taifa jirani la Afghanistan. Serikali ya Pakistan kwa upande wake imelaumu Marekani mara kadhaa kwa kuingilia anga yake na kudharau utawala kwa kukosa kushirikiana nayo katika mashambulizi hayo.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Hali ya mume wa Malkia inaimarika


Hali ya mume wa Malkia wa Uingereza "imeimarika" lakini anatarajiwa kuwepo hospitali katika siku chache zijazo, taarifa kutoka kwa Kasri ya Buckingham imesema.

Prince Philip mwenye umri wa miaka 90, amekuwa hospitali kwa siku mbili akitibiwa matatizo ya kibofu cha mkojo, na alikosa sherehe za mwisho za kuadhimisha miaka sitini ya utawala wa Malkia Elizabeth wa pili.

Msemaji wa Kasri ya Buckingham anasema Prince Philip "yuko katika hali nzuri".

Prince Philip alipelekwa hospitali siku ya Jumatatu, saa chache kabla ya tamasha la muziki lililofanyika nje ya Kasri ya Buckingham.

Anatibiwa katika hospitali ya Mfalme Edward wa saba katikati mwa London.

Msemaji wa kasri alisema: " Anaendelea na matibabu na anapewa dawa kwa sasa.

" Anatarajiwa kubaki hospitali katika siku chache zijazo. Yuko katika hali nzuri."

Siku ya Jumanne, mwanae mdogo wa kiume wa Malkia, alisema babake "yuko vizuri".
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

ZIMBABWE: MWANA AMJAZA MIMBA MAMAYAKE MARA MBILI

Chifu wa kijiji, Chinamhora, aliyetoa tamko la kukamatwa watu hao.

KATIKA tukio la aina yake, mwanaume mmoja na mama yake mzazi wamekuwa na uhusiano wa kimapenzi ambao umesababisha mwanamke huyo kupata mimba mara mbili. Simon Matsvara na Ethel Vhangare ni wakazi wa kijiji cha Pote.
Simon alimpa ujauzito mama yake wakati baba yake, Agripah Matsvara, alipokuwa hai, na akampa ujauzito mara ya pili baada ya kifo chake.
Mara ya kwaza ujauzito huo ulitoka, lakini wakati huu Vhangare anadaiwa kuwa na ujauzito wa miezi mitano alioupata kutoka kwa Simon.
Watu hao wanasemekana kuwa wamekimbia baada ya msako wa kuwakamata ulioamrishwa na Chifu.
Inasemekana mwaka 2008, Agripah, alipatwa na kiharusi ambapo wawili hao walisaidiana kumuuguza, lakini baadaye mama huyo akaanza kuwa anatapika na kuwaeleza majirani kwamba alikuwa mjamzito na mhusika ni mwanaye.
Wanafamilia wanasemekana waliwapiga faini kwa kuwaambia watoe n'gombe ambao idadi yake haikufahamika.
Hata hivyo, mwaka huo wa 2008, mimba ya Vhangare iliharibika kabla ya mumewe kufariki mwaka huohuo. Hata hivyo, Simon na mama yake waliendeleza uhusiano wao wa kimapenzi na mama huyo kupata mimba tena ambapo amri ya kuwakamata ilitolewa ili kuwaadhibu kwa kitendo hicho cha aibu.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

UKOSEFU WA USINGIZI NI HATARI KWA AFYA YAKO


KITENDO cha kukosa usingizi mara kwa mara wakati wa kulala kuna weza kuonekana ni jambo ambalo halina madhara kiafya, lakini ukweli ni kwamba unapokosa usingizi, hasa kwa muda mrefu, kuna athari kubwa katika afya yako yote, hata kama unakula na kufanya mazoezi vizuri.

Madhara ya ukosefu usingizi huathiri mfumo mzima wa mwili, mathalan, mbali ya kuathiri kinga ya mwili na kuongeza hatari ya kupatwa na magonjwa ya saratani, ukosefu wa usingizi huweza kusababisha madhara mengine yafutayo:

HATARI YA KUPATWA NA UGONJWA WA MOYO
Unapokosa usingizi, mfumo wa uzalishaji homoni huvurugika ambapo uzalishaji wa homoni za ‘stresi’ (stress hormones) huongezeka. Pia husababisha vidonda vya tumbo na hali ya kusikia njaa hata kama umetoka kula muda mfupi. Uko hatarini kusumbumbuliwa na hasira na ghadhabu kila mara.

ONGEZEKO LA SHINIKIZO LA DAMU
Ukosefu wa usingizi huchangia pia ongezeko la shinikizo la damu, pia huchangia kuzeeka kwa mtu kutokana na kuvurugika kwa uzalishaji wa homoni za ongezeko la umri. Humfanya mtu kuonekana mzee ili hali bado ana umri mdogo.

KUZIDISHA TATIZO LA UKOSEFU WA CHOO
Ukosefu wa usingizi huchangia pia tatizo la ukosefu wa choo na huweza hata kusababisha kifo kama tatizo likiwa sugu.

EPUKA KUTUMIA DAWA ZA USINGIZI
Kama unasumbuliwa na tatizo la ukosefu wa usingizi, jua kwamba hauko peke yako. Utafiti uliofanywa hivi karibuni nchini Marekani na Taasisi ya Taifa ya Usingizi (National Sleep Foundation –NSF), umegundua kuwa kati ya watu 10, ni wanne tu hupata usingizi mzuri kila wiki.
Pamoja na kuonekana kwa athari nyingi za kukosekana kwa usingizi, lakini utakuwa unajiweka katika madhara na hatari zaidi iwapo utalazimisha kupata usingizi kwa kumeza dawa za usingizi, kwa sababu ni hatari na mara nyingi dawa hizo huwa hazisaidii kuondoa tatizo.

JINSI YA KUFANYA ILI UPATE USINGIZI
Kwa asili yake, kichocheo cha usingizi mwilini kijulikanacho kama ‘melatonin’ hupatikana kwa ulaji wa mboga za majani na matunda mbalimbali ya kuongeza virutubisho mwilini na hupatikana pia kwa kupata mwanga wa jua wa kutosha wakati wa mchana. Hivyo huna haja ya kumeza vidonge badala yake zingatia uzalishaji wa kirutubisho hicho kwa mlo na mwanga wa jua.
Ili kujiwekea mazingira mazuri ya kupata usingizi mzuri, unashauriwa kuepuka kufanya yafuatayo muda mfupi kabla ya kupanda kitandani kulala:

Epuka kuangalia TV au kompyuta muda mfupi au saa moja kabla ya kulala, kwani teknolojia hizi siyo nzuri sana kwa macho kutokana na mwanga wake, hasa kwa mtu mwenye matatizo ya kupata usingizi.
Epuka kulala huku taa inawaka, hakikisha unalala huku taa zote zikiwa zimezimwa, licha ya mwanga wa taa usiku kusababisha madhara mengine, lakini huchangia kuharibu mtiririko wa usingizi. Hata uamkapo usiku kwenda msalani, ikiwezekana usiwashe taa ili kuepuka kuvuruga usingizi wako.
Usilale karibu na vifaa vya umeme na vyenye sumaku kama vile saa, simu, au redio kwani huchangia kudhoofisha uzalishaji wa homoni za usingizi. Hata saa yako yenye ‘alarm’ ya kukuamsha, unashauriwa kuiweka mbali nawe kabisa.

Mwisho, hakikisha unakuwa na ratiba ya kulala inayoeleweka na hakikisha unalala muda huohuo kila siku. Kwa kawaida mtu anatakiwa kulala kati ya saa tatu na saa nne usiku. Iwapo utazingatia vyote vilivyoelezwa hapo juu, bila shaka utaweza sasa kulala usingizi mnono.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
 

for more information call us

+255718953088
-------or-------
+255784953088
*email*
innocentfabian@gmail.com
THANKS

quote of the day

"Don't criticize me simply because I am different. Understand me, and you will most likely appreciate my difference and criticize your variance."