Social Icons

Saturday, October 12, 2013

MAPENZI YAMPOTEZA SKAINA

Stori: Brighton Masalu
STAA wa sinema za Kibongo, Skyner Ally ‘Skaina’ amepotea kwenye gemu chanzo kikidaiwa kuwa ni mapenzi kwani kila mwanaume anayeanzisha naye uhusiano wa kimapenzi, humzuia kuendelea kufanya kazi za sanaa.
‘Akibadilishana sentensi’ na mwandishi wetu, rafiki wa karibu wa msanii huyo ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini, alisema kitendo cha wanaume wengi wanaoanzisha uhusiano na Skaina kumzuia kuendelea na kazi ya uigizaji, kimechangia kumpoteza.
Mwandishi wetu ‘alipomvutia waya’ Skaina, aliambulia majibu ya ‘sintofahamu’ huku akisisitiza kutosumbuliwa.
“Sasa kama umeambiwa hivyo mnachoniuliza hapo ni nini? Kwani lazima niigize mara kwa mara? Mimi naipenda kazi yangu, sitaki maswali zaidi,” alisema Skaina.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

JACK DUSTAN AZURURA NUSU UTUPU DUBAI

Stori: Imelda Mtema
MREMBO aliyefahamika kupitia Shindano la Maisha Plus Season 2, Jacqueline Dustan, amenaswa akizururura mitaani na kibukta kifupi mithili ya nguo ya ndani.
Tukio hilo limetokea hivi karibuni pande za Dubai ambapo baada ya paparazi wetu kuzinyaka picha hizo, iliibuka minong’ono ya kulikoni avae hivyo wakati raia wengi wa huko wanavaa mavazi ya heshima.
Akichonga  na Weekly Star Exclusive, rafiki mkubwa wa Jacqueline ambaye hakupenda jina lake lichorwe gazetini ambaye ndiye aliyevujisha picha hizo,  alisema hata yeye alimshangaa sana shosti wake kwa kumtumia picha hizo.
“Sikuamiani kabisa kama ni yeye kwa maana sijawahi kumuona akivaa hivi huku Bongo japokuwa anavaa nguo fupi lakini siyo kama hicho kibukta alichokivaa na kukatiza mitaani bila wasiwasi wowote,” alisema rafiki huyo na kuongeza:
“Nilipojaribu kumuuliza kulikoni avae kikaptula hicho tena katika nchi za watu wanaojiheshimu, akadai kwake siyo ishu na zaidi ni Wabongo ndiyo wanaopenda kufuatilia maisha ya watu.”
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

WASTARA ASEMA KUOLEWA NI LAZIMA

Stori: Brighton Masalu
MWIGIZAJI mahiri Bongo, Wastara Juma Issa Abeid ‘Wastara’ amesema suala la kuolewa tena halikwepeki licha ya kutokuwa na mawazo juu ya suala hilo kwa sasa.
Akizungumza na paparazi wetu, Wastara ambaye ni nadra sana kukosea awapo mbele ya kamera, alisema yeye kama mwanamke aliyekamilika hadhani kama atakaa bila mwanaume lazima ataolewa tena.
“Mimi ni mwanamke niliyekamilika, suala la kuolewa ni lazima, japo kwa sasa sifikirii kufanya hivyo, lakini sidhani kama nitaweza kukaa bila mwanaume, lakini pia usumbufu kutoka kwao unaendelea,” alisema Wastara
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

MIMBA ROSE NDAUKA YAWA KIVUTIO...

Na Imelda Mtema
MUONEKANO mpya wa ‘kubugia kijusi’ wa msanii wa filamu za Kibongo, Rose Donatus Anjelus Ndauka ‘mtata’ umezua miguno, minong’ono huku ikionekana kivutio kwa wengi na kubaki wakihoji maswali yasiyojibika haraka, Risasi Jumamosi linaifunua.
Hayo yalichukua nafasi hivi karibuni wakati staa huyo alipofanya sherehe ya kutimiza miaka kadhaa tangu ‘anuse hewa ya Oksijeni’ iliyofanyika ndani ya ukumbi wa Club Escape Beach Kigamboni jijini Dar na kuacha historia ya aina yake.
Baadhi ya wahudhuriaji wa sherehe hiyo, walionekana kuwa na viulizo vingi juu ya mimba yake, huku gauni fupi alilovaa siku hiyo likiionesha kwa ufasaha mimba hiyo na kufanya baadhi yao kubaki wasiamini kama kweli msanii huyo amechukua uamuzi wa kuzaa kabla ya ndoa.
“Mh! hivi kweli Rose ana mimba?, siamini kama ameamua kuzaa kabla ya ndoa si alikuwa akikataa huyu? Sasa imekuwaje” alisikika mama mmoja katika sherehe hiyo.
“Ila kapendeza jamani, sasa kaonekana mwanamke kweli,  muone anavyotembea kwa madaha, mimba hiyo imemuongezea mvuto!” alisema msanii mwingine wa kike mwenye ‘taito’ kubwa bongo.
Mwandishi wetu alipomuuliza Rose juu ya minong’ono hiyo, alijibu kwa kifupi huku akionekana kufurahia.
“Jamani sina jibu la kuwapa, kama watu wanashangaa ni wao niseme nini tena?” alisema Rose na kisha kufunga ‘faili’ la mazungumzo na mwandishi wetu.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

SNURA: SIKATI MAUNO ILI NIIBE WANAUME

Stori: Mayasa Mariwata
STAA wa Majanga, Snura Antony Mushi ‘Snura’ amesema kamwe wanaume za watu wasimmendee katika shoo zake kwani hakati mauno ili kuwapata hasa wenye wake.
Akipiga stori na paparazi wetu, Snura alisema kukata mauno kwenye shoo ndiyo silaha yake ya kuwateka mashabiki lakini anashangaa kuona wanaume za watu ndiyo wanaongoza kwa kutuma maombi ya kutongoza.
“Sipendi kabisa kusikia masuala ya wanaume za watu, siko tayari kuvunja ndoa za watu. Pesa za kuhongwa sioni raha nazo hata kidogo napenda za kujitafutia za kwangu,” alisema Snura.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Friday, October 11, 2013

UMEIONA TATOO MPYA YA LULU? KAMA BADO ICHEKI HAPA IMEANDIKWA "ONLY GOD CAN JUDGE ME"




O yes "ONLY GOD CAN JUDGE ME."
 
credits :jestina george
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

KUHONGWA KWA LINAH KWAIBUA MAMBO

Na Mwandishi Wetu
MAELEZO ya hivi karibuni aliyodaiwa kuyatoa mwanamuziki Estelina Sanga ‘Linah’ mtandaoni kuwa mtaji wake katika kazi za ujasiriamali ameupata kwa kuhongwa na mpenzi wake na kuchanganya na pesa zake yameibua mambo.
Wakionesha kushangazwa kwao na maelezo hayo, baadhi ya mashabiki wake walisema kitendo cha yeye kukiri kuwa anahongwa kinawashawishi wasichana wengine wahisi nao bila kuhongwa hawawezi kufanikiwa.
“Huyu anasema mtaji wake ameupata kwa kuhongwa na mpenzi wake, ina maana asingehongwa asingefika hapo alipo? Na sisi tutafute wa kutuhonga ili tufanikiwe? Lakini kwani mpenzi wako akikupa pesa anakuhonga? Linah asitupotoshe,” alisema Neema Kiza.
Mdau mwingine ambaye hakupenda kutaja jina lake alisema: “Eti anasema amehongwa na mpenzi wake, sasa anatuambia ili iweje? Hata hivyo, mpenzi wako anapokupa pesa hakuhongi, anakusaidia, alijue hilo.”
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
 

for more information call us

+255718953088
-------or-------
+255784953088
*email*
innocentfabian@gmail.com
THANKS

quote of the day

"Don't criticize me simply because I am different. Understand me, and you will most likely appreciate my difference and criticize your variance."