IKIWA utaosha nywele zako kama kawaida na baadaye kutumia chanuo ama 
brash katika kuzibana, wakati mwingine unaweza kusababisha kukatika au 
hata kuathiri ukuaji wa nywele zako.
 Hata hivyo, kwa kufuata ushauri unaweza kuepukana na tatizo hilo na 
hivyo kusababisha nywele zako kujaa na kukua vyema.  Fuata hizi dondoo 
rahisi ambazo ili kuhakikisha unasaidia sio kuua nywele zako bali 
kuzikuza na kuzifanya zinawiri. Ikiwa unatumia mafuta ya jeli, umakini 
unahitajika katika kuziosha nywele zako. Kama unatumia jeli ya nywele 
katika mtindo wako, hakikisha unaosha vizuri na kuondoa jeli yote kabla 
ya  kulala. Unapolala na jeli au urembo mwingine unaofanana nayo, 
unasababisha kuziba kwa tundu za nywele katika ngozi ya kichwa.
 Kitendo hicho mbali na kuzuia kupumua kwa ngozi ya kichwa pia huchangia
 kuzuia nywele chipukizi kuota katika ngozi ya kichwa. Kuwa makini na 
shampoo za madukani Mara nyingi baadhi ya watengenezaji wa vipodozi 
huweka maslahi mbele bila kuangalia athari zinazoweza kuwapata watumiaji
 wa bidhaa zao. Kwani kuna baadhi ya shampoo huwa na kemikali hatari kwa
 ngozi. Hivyo ni vyema zaidi ikiwa utakuwa na uelewa wa kutosha 
kuhusiana na aina hiyo ya kipodozi. Pendelea zaidi kutumia herbal 
shampoo.
 Si hivyo tu wakati mwingine vipodozi vya bei rahisi huwa na kasoro, 
hivyo ni vyema kupata ushauri kutoka kwa wataalamu wa nywele kujua ni 
aina gani ya shampoo ni sahihi kwa nywele zako. Kinyume cha hapo unaweza
 kuishia kuathiri nywele na ngozi yako bila ya mwenyewe kufahamu. Epuka 
kubana nywele mara kwa mara Ubanaji wa nywele hasa kuelekea mgongoni 
mara nyingi huhatarisha maisha ya nywele zako hasa za usoni. Kwani 
kiteno cha kuzibana husababisha kuvutwa kwa nywele na hivyo kusabisha 
kukatika hasa kwa zile zilizo hafifu.
 Usichane nywele zikiwa mbichi Zinapokuwa mbichi nywele huwa na 
uwezekano mkubwa wa kukatika hasa pale zinapochanwa au kufutwa kwa taulo
 gumu. Ni vyema ukaacha zikauke kwa upepo na baada ya hapo unaweza 
kuzichana. Katika hili kama utakuwa unatumia ‘conditioner’hakikisha 
husugui katika nywele na badala yake tumia kwa kupaka. Ikiwa kama nywele
 zako zimekatika na hazilingani, ni vyema ukakata ncha ili 
kuzisawazisha. Hii husaidia kuzifanya zikue vizuri na pia kuondoa 
uwezekano wa kukatika mara zinapoingia maji. 
Hasa kwa zile zenye ‘relaxer’.   Chochea ukuaji wa nywele zako kwa 
kuzichana Unapochana nywele zako hakikisha unatumia shanuo la mbao au 
kitana chenye meno yaliyoachana. Hakikisha nywele zako zinakuwa kavu. 
Usizivute sana kwani pamoja kusababisha maumivu pia huleta uwezekano wa 
kukatika. 
 Jambo la muhimu katika uchanaji wa nywele, husaidia kuchochea mzunguko 
wa damu katika ngozi ya kichwa na pia husaidia kukua kwa nywele. 
Imarisha umaridadi wa nywele zako IKIWA utaosha nywele zako kama kawaida
 na baadaye kutumia chanuo ama brash katika kuzibana, wakati mwingine 
unaweza kusababisha kukatika au hata kuathiri ukuaji wa nywele zako
. Hata hivyo, kwa kufuata ushauri unaweza kuepukana na tatizo hilo na 
hivyo kusababisha nywele zako kujaa na kukua vyema.  Fuata hizi dondoo 
rahisi ambazo ili kuhakikisha unasaidia sio kuua nywele zako bali 
kuzikuza na kuzifanya zinawiri. Ikiwa unatumia mafuta ya jeli, umakini 
unahitajika katika kuziosha nywele zako. Kama unatumia jeli ya nywele 
katika mtindo wako, hakikisha unaosha vizuri na kuondoa jeli yote kabla 
ya  kulala. Unapolala na jeli au urembo mwingine unaofanana nayo, 
unasababisha kuziba kwa tundu za nywele katika ngozi ya kichwa.
 Kitendo hicho mbali na kuzuia kupumua kwa ngozi ya kichwa pia huchangia
 kuzuia nywele chipukizi kuota katika ngozi ya kichwa. Kuwa makini na 
shampoo za madukani Mara nyingi baadhi ya watengenezaji wa vipodozi 
huweka maslahi mbele bila kuangalia athari zinazoweza kuwapata watumiaji
 wa bidhaa zao. Kwani kuna baadhi ya shampoo huwa na kemikali hatari kwa
 ngozi. Hivyo ni vyema zaidi ikiwa utakuwa na uelewa wa kutosha 
kuhusiana na aina hiyo ya kipodozi. Pendelea zaidi kutumia herbal 
shampoo. Si hivyo tu wakati mwingine vipodozi vya bei rahisi huwa na 
kasoro, hivyo ni vyema kupata ushauri kutoka kwa wataalamu wa nywele 
kujua ni aina gani ya shampoo ni sahihi kwa nywele zako. Kinyume cha 
hapo unaweza kuishia kuathiri nywele na ngozi yako bila ya mwenyewe 
kufahamu. Epuka kubana nywele mara kwa mara Ubanaji wa nywele hasa 
kuelekea mgongoni mara nyingi huhatarisha maisha ya nywele zako hasa za 
usoni.
 Kwani kiteno cha kuzibana husababisha kuvutwa kwa nywele na hivyo 
kusabisha kukatika hasa kwa zile zilizo hafifu. Usichane nywele zikiwa 
mbichi Zinapokuwa mbichi nywele huwa na uwezekano mkubwa wa kukatika 
hasa pale zinapochanwa au kufutwa kwa taulo gumu. Ni vyema ukaacha 
zikauke kwa upepo na baada ya hapo unaweza kuzichana. Katika hili kama 
utakuwa unatumia ‘conditioner’hakikisha husugui katika nywele na badala 
yake tumia kwa kupaka. Ikiwa kama nywele zako zimekatika na hazilingani,
 ni vyema ukakata ncha ili kuzisawazisha. Hii husaidia kuzifanya zikue 
vizuri na pia kuondoa uwezekano wa kukatika mara zinapoingia maji. Hasa 
kwa zile zenye ‘relaxer’.   Chochea ukuaji wa nywele zako kwa kuzichana 
Unapochana nywele zako hakikisha unatumia shanuo la mbao au kitana 
chenye meno yaliyoachana.
 Hakikisha nywele zako zinakuwa kavu. Usizivute sana kwani pamoja 
kusababisha maumivu pia huleta uwezekano wa kukatika.  Jambo la muhimu 
katika uchanaji wa nywele, husaidia kuchochea mzunguko wa damu katika 
ngozi ya kichwa na pia husaidia kukua kwa nywele
 TOA MAONI YAKO HAPA CHINI