Social Icons

Friday, October 11, 2013

KUHONGWA KWA LINAH KWAIBUA MAMBO

Na Mwandishi Wetu
MAELEZO ya hivi karibuni aliyodaiwa kuyatoa mwanamuziki Estelina Sanga ‘Linah’ mtandaoni kuwa mtaji wake katika kazi za ujasiriamali ameupata kwa kuhongwa na mpenzi wake na kuchanganya na pesa zake yameibua mambo.
Wakionesha kushangazwa kwao na maelezo hayo, baadhi ya mashabiki wake walisema kitendo cha yeye kukiri kuwa anahongwa kinawashawishi wasichana wengine wahisi nao bila kuhongwa hawawezi kufanikiwa.
“Huyu anasema mtaji wake ameupata kwa kuhongwa na mpenzi wake, ina maana asingehongwa asingefika hapo alipo? Na sisi tutafute wa kutuhonga ili tufanikiwe? Lakini kwani mpenzi wako akikupa pesa anakuhonga? Linah asitupotoshe,” alisema Neema Kiza.
Mdau mwingine ambaye hakupenda kutaja jina lake alisema: “Eti anasema amehongwa na mpenzi wake, sasa anatuambia ili iweje? Hata hivyo, mpenzi wako anapokupa pesa hakuhongi, anakusaidia, alijue hilo.”
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

No comments:

Post a Comment

 

for more information call us

+255718953088
-------or-------
+255784953088
*email*
innocentfabian@gmail.com
THANKS

quote of the day

"Don't criticize me simply because I am different. Understand me, and you will most likely appreciate my difference and criticize your variance."