Social Icons

Saturday, October 12, 2013

JACK DUSTAN AZURURA NUSU UTUPU DUBAI

Stori: Imelda Mtema
MREMBO aliyefahamika kupitia Shindano la Maisha Plus Season 2, Jacqueline Dustan, amenaswa akizururura mitaani na kibukta kifupi mithili ya nguo ya ndani.
Tukio hilo limetokea hivi karibuni pande za Dubai ambapo baada ya paparazi wetu kuzinyaka picha hizo, iliibuka minong’ono ya kulikoni avae hivyo wakati raia wengi wa huko wanavaa mavazi ya heshima.
Akichonga  na Weekly Star Exclusive, rafiki mkubwa wa Jacqueline ambaye hakupenda jina lake lichorwe gazetini ambaye ndiye aliyevujisha picha hizo,  alisema hata yeye alimshangaa sana shosti wake kwa kumtumia picha hizo.
“Sikuamiani kabisa kama ni yeye kwa maana sijawahi kumuona akivaa hivi huku Bongo japokuwa anavaa nguo fupi lakini siyo kama hicho kibukta alichokivaa na kukatiza mitaani bila wasiwasi wowote,” alisema rafiki huyo na kuongeza:
“Nilipojaribu kumuuliza kulikoni avae kikaptula hicho tena katika nchi za watu wanaojiheshimu, akadai kwake siyo ishu na zaidi ni Wabongo ndiyo wanaopenda kufuatilia maisha ya watu.”
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

No comments:

Post a Comment

 

for more information call us

+255718953088
-------or-------
+255784953088
*email*
innocentfabian@gmail.com
THANKS

quote of the day

"Don't criticize me simply because I am different. Understand me, and you will most likely appreciate my difference and criticize your variance."