Social Icons

Saturday, October 12, 2013

MAPENZI YAMPOTEZA SKAINA

Stori: Brighton Masalu
STAA wa sinema za Kibongo, Skyner Ally ‘Skaina’ amepotea kwenye gemu chanzo kikidaiwa kuwa ni mapenzi kwani kila mwanaume anayeanzisha naye uhusiano wa kimapenzi, humzuia kuendelea kufanya kazi za sanaa.
‘Akibadilishana sentensi’ na mwandishi wetu, rafiki wa karibu wa msanii huyo ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini, alisema kitendo cha wanaume wengi wanaoanzisha uhusiano na Skaina kumzuia kuendelea na kazi ya uigizaji, kimechangia kumpoteza.
Mwandishi wetu ‘alipomvutia waya’ Skaina, aliambulia majibu ya ‘sintofahamu’ huku akisisitiza kutosumbuliwa.
“Sasa kama umeambiwa hivyo mnachoniuliza hapo ni nini? Kwani lazima niigize mara kwa mara? Mimi naipenda kazi yangu, sitaki maswali zaidi,” alisema Skaina.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

No comments:

Post a Comment

 

for more information call us

+255718953088
-------or-------
+255784953088
*email*
innocentfabian@gmail.com
THANKS

quote of the day

"Don't criticize me simply because I am different. Understand me, and you will most likely appreciate my difference and criticize your variance."