Social Icons

Thursday, June 7, 2012

DAR INATISHA


JIJI la Dar es Salaam na viunga vyake hasa maeneo ya maegesho ya magari (parking), viwanja vya wazi na ufukweni, linatisha kwa vitendo vya ngono za rejareja vikiongozwa na watu maarufu, Amani limefanya uchunguzi wake na hii ndiyo ripoti kamili.
Kwa nyakati tofauti, hivi karibuni, gazeti hili lilinasa matukio yenye kutia kinyaa yakifanywa waziwazi na wakati mwingine mchana kweupe.
Katika maeneo tofauti, kamera yetu iliwanasa mabinti wadogo ‘wakidendeka’ hadharani bila kujali umati uliowazunguka.

MAENEO HATARINI
Maeneo yanayotajwa kukithiri kwa uchafu huo jijini Dar ni pamoja kwenye mikusanyiko ya wazi kama Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni Makaburini, Buguruni, Ufukwe wa Coco na kwenye ‘parking’ mbalimbali za kumbi za starehe.

NDANI YA LEADERS
Mabinti waliotambuliwa kwa jina mojamoja, Husna na Vai walinaswa kwenye Viwanja vya Leaders Club wakifanya matendo machafu ya kisagaji.





MLIMANI CITY
Jumapili moja, Amani likiwa ‘rovingi’ liliwamulika ‘masistaduu’ ambao walitajwa kwa jina mojamoja, Jack na Teddy kwenye ‘parking’ za Mlimani City ambao wanadaiwa kuwa miongoni mwa kundi la wadada wanaoligeuza Jiji la Dar kuwa kama Sodoma na Gomora kwa kujihusisha na vitendo vichafu vya ngono.

COCO BEACH
Pia ‘patroo’ yetu ilimtia kibindoni mwigizaji wa muvi za Kibongo, Isabela Francis ‘Vai wa Ukweli’ ‘akidendeka’ na mwanaume aliyedaiwa kuwa ni ‘kuku mtamu’ kwenye Ufukwe wa Coco.

MANGO GARDEN
Kwenye Ukumbi wa Mango Garden, demu aliyetajwa kwa jina moja la Jack naye aliingia mtegoni baada ya kunaswa akiwalegezea zipu wanaume bila kujali macho ya kadamnasi.

FUKWE ZA BAGAMOYO
Mbali na maeneo hayo, pia fukwe nyingi zinazoanzia Dar hadi Bagamoyo nazo zilifumuliwa na ‘shushushu’ wetu aliyeshudia uchafu wa ajabu wa ngono rejareja zikihusisha dada zetu na watasha.




WAZAZI
Dawati la Amani linatumia fursa hii kuwataka wazazi kuwatupia macho watoto wao hasa mabinti kwani hali ni mbaya na watachuma majanga muda si mrefu.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

No comments:

Post a Comment

 

for more information call us

+255718953088
-------or-------
+255784953088
*email*
innocentfabian@gmail.com
THANKS

quote of the day

"Don't criticize me simply because I am different. Understand me, and you will most likely appreciate my difference and criticize your variance."