Social Icons

Thursday, April 25, 2013

KIDUMU AMMWAGA MZAZI MWENZIYE

Stori: Sophia Marcel
MWANAMUZIKI kiwango wa Burundi anayepiga mzigo pande za Kenya, Nimbona Jean Pierre ‘Kidumu’ amemwagana na mzazi mwenzake aliyezaa naye watoto wawili.
Kwa mujibu wa chanzo makini, Kidumu ameamua kuachana na mwanamke huyo aliyekuwa akiishi naye awali baada ya kupata kifaa kipya kinachosoma Chuo Kikuu cha Nairobi ambacho anatarajia kufunga nacho pingu za maisha Julai, mwaka huu.
Alipoulizwa na waandishi kuhusiana na ishu hiyo, Kidumu alikiri kumpata mpenzi huyo mpya toka kabila la Wakikuyu na kubainisha kuwa ndiye anayemlelea watoto wake ambao alizaa na mwanamke wake wa awali ambaye hakumtaja jina.
“Ni mapema kumjua kwa jina mpenzi wangu mpya, mashabiki wajue kwamba ninaye na nitawatambulisha mambo yatakapokuwa sawa huko mbeleni,” alisema Kidumu.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

No comments:

Post a Comment

 

for more information call us

+255718953088
-------or-------
+255784953088
*email*
innocentfabian@gmail.com
THANKS

quote of the day

"Don't criticize me simply because I am different. Understand me, and you will most likely appreciate my difference and criticize your variance."