Social Icons

Friday, April 26, 2013

USHOSTI WA LULU, PENNY WAZUA MINONG’ONO

Stori:Hamida Hassan
Ushosti unaoonekana kuwepo sasa kati ya msanii wa filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’ na Mtangazaji wa Kituo cha Televisheni cha DTV ambaye ni mpenzi wa mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’,  Penniel Mungilwa ‘Penny’ umeibua minong’ono huku baadhi wakidai eti Lulu ana lengo la kumrusha roho Wema.
Hilo limeibuka kutokana na ukweli kwamba, sasa hivi Wema na Penny haziivi baada ya Diamond kuhamishia penzi kwa mtangazaji huyo na kwamba kitendo cha Lulu kuonekana ‘close’ sana na Penny ni lazima kitamuuma Wema.
“Ni ukweli ulio wazi kuwa Wema hawezi kumpenda Penny, lakini pia kitendo cha Lulu kuwa karibu na Penny ni lazima kitamuuma Wema na atahisi lao ni moja, inawezekana Lulu kafanya makusudi ili kumrusha roho Wema,” alisema msanii mmoja wa filamu aliyeomba hifadhi ya jina lake kukwepa bifu.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

No comments:

Post a Comment

 

for more information call us

+255718953088
-------or-------
+255784953088
*email*
innocentfabian@gmail.com
THANKS

quote of the day

"Don't criticize me simply because I am different. Understand me, and you will most likely appreciate my difference and criticize your variance."