Social Icons

Thursday, April 25, 2013

MZEE KANKAA AGONGWA NA GARI

Stori:Denis Mtima ma Chande Abdallah
MSANII mkongwe wa filamu Bongo, Juma Ally Salim ‘Mzee Kankaa’ amegongwa na gari wakati akifanya mazoezi ya kutembea kufuatia ugonjwa wake wa kiharusi.
Tukio hilo lilitokea Aprili 21, mwaka huu maeneo ya Kariakoo, Dar ambapo gari hilo aina ya Toyota Voxy lilitokea ghafla na kumgonga kidogo na kumsababishia michubuko kwenye miguuni na kichwani.
Dereva wa gari hilo alifanya uungwana kwa kumpeleka katika Kituo cha Polisi cha Msimbazi ambapo ndugu zake walitaarifiwa na kwenda kumchukua.
“Mzee Kankaa alitoka nyumbani na kutuaga kuwa anakwenda kufanya matembezi. Tulijua ni karibu, lakini baadaye tukasikia taarifa kuwa amepata ajali na yupo Kituo cha Polisi Msimbazi,” alisema Abdul ambaye ni mtoto wa Kankaa.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

No comments:

Post a Comment

 

for more information call us

+255718953088
-------or-------
+255784953088
*email*
innocentfabian@gmail.com
THANKS

quote of the day

"Don't criticize me simply because I am different. Understand me, and you will most likely appreciate my difference and criticize your variance."