Social Icons

Thursday, April 25, 2013

IRENE UWOYA: UKINIPASUA ROHONI UTAMUONA KRISH

Stori:Imelda Mtema
MAMBO vipi msomaji wangu wa safu hii maridhawa ya Staa na Mwana, kama ilivyo ada hapa tunapata kuwajua watoto wa mastaa.
Big up kwenu ambao mnaendelea kutuma maoni yenu, nawashukuru sana. Kutokana na maombi ya wengi, leo tunaye mwigizaji, Irene Uwoya ambaye ni mama wa mtoto mmoja, Krish Ndikumana.
Birthday Boy Krish akiwa katika pose siku ya bethidei yake mwaka jana
Krishi ana umri wa miaka miwili, ili kujua mengi ungana nami katika mahojiano niliyofanya naye hapa chini:
Krish na mama yake wakizima mishumaa wakati wa bethidei yake mwaka jana
KRISH NDIYO NUSU  YA MAISHA YAKE
“Ki ukweli nafikiri kabisa mtoto wangu ndiyo nusu ya maisha yangu, ukinipasua roho yangu utamkuta yeye na ninaweza kutembea lakini nikimkumbuka tu, akili yangu inafikiria kumuona wakati huohuo.”
NINI MAANA YA JINA LA KRISH
“Kuna filamu ya Kihindi nilikuwa nikiipenda sana kuitazama ilikuwa ikiitwa Krish, kwa kweli nilijiwekea nadhiri kuwa kama nikibahatika kujifungua mtoto wa kiume nitampa jina la Krish na Mungu aliponibariki nikafanya hivyo.”
UPENDO KWA MTOTO UPOJE?
“Kiukweli nahisi Krish ndiyo mtu wa kwanza ninayempenda katika uso wa dunia na wengine wanafuata kwa sababu kuna wakati nahisi ni kama nyama yangu imekatwa halafu akatokea Krish.”
ANAISHI NAYE?
“Krish tangu nijifungue anaishi kwa bibi yake na amezoea sana huko, hata bibi na babu yake wanapenda sana kukaa naye kwa vile ni mjuu wao wa kwanza hivyo kwao ndiyo kila kitu.”
HAMKUMBUKI MWANAYE?
“Daah! Unajua kuna wakati najishangaa iwe usiku kiasi gani, nikimkumbuka mwanangu nawasha gari hadi Mbezi fasta nakwenda kumuona na nyumbani huwa wanashangaa sana.”
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

No comments:

Post a Comment

 

for more information call us

+255718953088
-------or-------
+255784953088
*email*
innocentfabian@gmail.com
THANKS

quote of the day

"Don't criticize me simply because I am different. Understand me, and you will most likely appreciate my difference and criticize your variance."