Social Icons

Thursday, May 16, 2013

AUNT EZEKIEL APOZWA MACHUNGU YA MAREHEMU MAMA’KE NA MTOTO WA KAKA’KE


Na Imelda Mtema
ALHAMISI nyingine imewadia msomaji wangu, tunakutana tena na mastaa ambao Mungu amewajilia kupata mtoto na kujua staili wanayoishi nyumbani kwao.
Aunt Ezekiel 'Mrs Demonte' akiwa na 'mwanaye' Nicole.
Leo tunaye staa wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel 'Mrs Demonte' ambaye anaishi maeneo ya Mwananyamala, jijini Dar na mtoto wa miaka 2 anaiyetwa Nicole kama mwanaye wa kumzaa.
Hivyo basi, kutokana na kumlea mtoto huyo tangu akiwa mdogo, moja kwa moja amepata nafasi ya kukaa kwenye safu hii, ungana nami katika mahojiano niliyofanya naye;
Amani: Mambo vipi, mtoto huyo kila siku uko naye ni wa nani?
Aunt: (kicheko cha kiana) Ni wangu, watu wanafikiri mimi sina mtoto?
Amani: Hata mimi ndiyo najua leo, ulimzaa kwa siri?
Nicole akimlisha keki 'mama'ke'.
Aunt: Hapana bwana nilikuwa nakutania tu, huyu ni mtoto wa kaka yangu.
Amani: Mh! Mbona kila nikikutembelea hapa kwako nakuona uko naye, wazazi wake wapo wapi sasa?
Aunt: Wazazi wake wote wapo lakini mtoto huyu ni zaidi ya kila kitu kwangu.
Amani:  Kivipi?
Aunt: Yaani tangu anazaliwa yuko mikononi mwangu na nikaamua kumlea mimi kama mtoto wangu na hata yeye anajua mimi ni mama yake mzazi.
Amani: Kwani ndugu zako si wana watoto wengi, kwa nini huyu tu?
Aunt: Huyu ni mtoto wa kaka yangu ambaye kwa mama yetu tulizaliwa wawili tu hivyo nikimuona huwa ananipoza machungu kwani ni kama marehemu mama yangu.
Nicole katika pozi.
Amani: Sasa unavyosafiri kwenda Dubai kwa mumeo huwa inakuwaje?
Aunt: Yaani huwa ninamkumbuka sana na nikimuona mtoto amekatiza mbele yangu huwa naumia na machozi kunilengalenga kabisa.
Amani: Sasa kwa nini usiondoke naye?
Aunt: Ndiyo nimeanza kufanya taratibu hizo maana hata shule nimemtafutia kule Dubai.
Amani: Sasa vipi Mungu akikujalia mtoto wako, upendo utazidi kuendelea kwa huyu au vipi?
Aunt: Nitawapenda wote, sidhani kama kutakuwa na tofauti kati ya mwanangu na huyu kwa sababu nampenda sana Nicole.
Amani: Nashukuru sana Aunt.
Aunt: Asante, karibu tena.
Upendo wa mama na mwana.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

No comments:

Post a Comment

 

for more information call us

+255718953088
-------or-------
+255784953088
*email*
innocentfabian@gmail.com
THANKS

quote of the day

"Don't criticize me simply because I am different. Understand me, and you will most likely appreciate my difference and criticize your variance."