Social Icons

Thursday, May 9, 2013

DEREVA AZIMIKA BARABARANI

Na Gladness Mallya
MWANAUME mmoja aliyetambulika kwa jina la Joseph Mwaleni anayedaiwa kuwa ni dereva wa kituo kimoja cha redio Bongo (jina tunalihifadhi), alikutwa amezimika ghafla na kuuchapa uzingizi barabarani akiwa kwenye gari lake.
Dereva Joseph Mwaleni akiwa amezima ndani ya gari alilokuwa anaendesha maeneo ya Sinza-Afrikasana.
Ishu hiyo ilitokea wikiendi iliyopita maeneo ya Sinza-Afrikasana ambapo Joseph akiwa kwenye foleni alipitiwa na usingizi mzito na magari yalipoanza kutembea gari lake liliendelea kusimama hali iliyosababisha foleni kuwa kubwa ndipo walipotokea wasamaria wema wakalisukuma mpaka pembeni huku njemba huyo akiwa amelala fofofo.
Gari alilokuwa anaendesha Joseph.
Baada ya kusogezwa pembeni, msamaria mwema alimpekua mifukoni, akachukua simu yake na kumpigia mmoja wa watu aliowasevu ambaye alifika eneo la tukio na ndiye alitoa maelezo kuwa jamaa huyo alikuwa dereva wa kituo hicho cha redio.
“Huyu jamaa amelewa kupitiliza kwanza ukimnusa hivi unasikia harufu ya pombe tu, tumemtoa katikati ya barabara na amshukuru Mungu kwa sababu amekutana na sisi wasamaria wema,” alisema shuhuda mmoja.
Dereva Joseph Mwaleni akiwa hoi ndani ya gari.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

No comments:

Post a Comment

 

for more information call us

+255718953088
-------or-------
+255784953088
*email*
innocentfabian@gmail.com
THANKS

quote of the day

"Don't criticize me simply because I am different. Understand me, and you will most likely appreciate my difference and criticize your variance."