Social Icons

Thursday, May 9, 2013

HUYU NDIO PRODUCER WA MUZIKI KUTOKA MWANZA, AMBAYE MSANII AKILETA MZAHA KAZINI ANAMCHAPA VIBOKO

Discipline, Discipline, Discipline! Ndo neno ambalo wengi wanalisisitiza katika kila kitu, lakini kwa Producer wa hit song ya Belle 9 ‘Listen’ Tiddy Hotter wa One Love FX iliyoko jijini Mwanza inaweza kuwa na uzito zaidi ya jinsi mwingine anavyoweza kulichukulia.


Surprisingly, Producer huyu hutumia viboko kuirejesha discipline studio kwa wasanii wanapungukiwa ama kukosa kabisa discipline wakiwa wanarekodi.


Hahahah, hiki ndio kiboko anachotumia Tiddy awapo studio, it's funny right?
Katika interview aliyofanya na MilazO 101 ya Radio One, Tidd Hotter  alipoulizwa alikiri kuwatandika mboko a.k.a bakora wasanii akiwa studio, lakini alisema sio kwa ubaya ni kwa uzuri na kwa urafiki tu.

“hahahaaa..yeah, unajua hiyo inatokana na baadhi ya wasanii wanapokuwa hawako serious, unajua kuna kukosea kwa aina nyingi, mtu anaweza kukosea kwamba kweli akili yake iko mbali na ukweli anaohitaji kuujua kwa muda ule, na kuna mwingine  unaona kabisa anahitaji tu juhudi flani kuliko matani, kwa hiyo wengine wanaleta matani kidogo na hiyo ni kazi yangu sa inabidi twende sawa kidogo ili kumfanya a-concentrate, unajua kiboko ni kitu kizuri kinachomfanya mtu a-concentrate kwenye kazi, sio kwa ubaya ni kwa urafiki tu kwa sababu baada ya hapo mnacheka tu vizuri..yeah.”

Inawezekana ukajiuliza labda jamaa anaitumia adhabu hii kwa wasanii wa aina gani, ambao wako chini yake ama yeyote, jamaa anafunguka.

“ni yeyote tu, kwa mfano kuna muda mwingine huwa na project za kwaya, labda tunarekodi nyimbo nyingi halafu inafika usiku, unakuta kuna wakina mama wenye umri mkubwa kabisa hata wanaweza kunizaa, wanakuwa wanalala wakati wa vocal. Kwa hiyo kiboko ni kitu ambacho nakitumia kumuamsha mtu awe kwenye ileee….”

Talking about umri wao, “Nawachapa wamama wakubwa sana, miaka hata wanafika 40, 50..wapo ambao wanalala wakati wa vocal, so napowapitishia viboko ..tah tah taaah…wanaendelea, kwa hiyo inasababisha mtu anaconcentrate..siwachapi niwaumize, na hata napokuwa nachapa siwachapi kama watoto wa shule niwachape niwaumize, yani ni kwa ajili tu ya kushtua, yan kuwagugusa watu kwenye brain, basi kitu kama hicho.

Tiddy aliulizwa, Wapo wasanii wengi wakubwa ambao jamaa ameshafanya nao kazi kama Belle9, Hardmad, Dark Master, Joslin, Dudu Baya na wengine wengi ambao wanafanya nae kazi ,je kuna mmoja kati yao alishawahi kukutana na adhabu hiyo(bakora).

“Yaani hao kwa sababu walishazoea na wanaijua game siku nyingi na experience yao ni kubwa najikuta siwezi kutumia hiyo njia, lakini natumia hiyo njia kwa sababu kuna wasanii wengine wanaichukulia kazi hii ya muziki kama sijui wanafanya nini?! Kwa hiyo anajikuta anaingiza mawazo mengine kwenye muziki. Kwa hiyo kakiboko kale ka mgongo kanasababisha mtu anakuwa sasa ah..kumbe nafanya kitu flani. So badala ya kutumia bangi au pombe ama nini mtu unamshtua brain yake na kuconcentrate kwenye kitu kwa kumuonesha kuwa kuna ka kiboko hapa..hahahahaa.”

Tiddy Hotter alimaliza kwa kusema Discipline ya mtu inamsababisha mtu kuwa mtu kwenye kile kitu anachokifanya.

msikilize Tiddy hotter
  msikilize Ben Pol pia akiongelea Nidhamu katika kazi:
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

No comments:

Post a Comment

 

for more information call us

+255718953088
-------or-------
+255784953088
*email*
innocentfabian@gmail.com
THANKS

quote of the day

"Don't criticize me simply because I am different. Understand me, and you will most likely appreciate my difference and criticize your variance."