Social Icons

Friday, May 3, 2013

WEMA AJINUNULIA MASHINE YA ‘MASAJI’

Na Imelda Mtema
BEAUTIFUL Onyinye wa Bongo, Wema Sepetu amejinunulia mtambo wa kufanyia masaji kwa lengo la kuondoa uchovu anaporejea nyumbani kwake akiwa amechoka.
Wema Sepetu.
Chanzo chetu makini kililitonya gazeti hili kuwa, kifaa alichonunua staa huyo ni mfano wa kiti ambacho mtumiaji anakaa na kukiseti anavyota kisha kinamuondoshea uchovu alionao.
“Yaani pale kwa Wema ukienda na uchovu wako unapelekwa kwenye kile kiti, wewe kazi yako unakaa tu na rimoti, unachagua ni wapi kikuweke sawa,” kilisema chanzo hicho.
Wema alipopigiwa simu na paparazi wetu kisha kuulizwa kuhusu kifaa hicho alikiri kukinunua na kueleza kuwa, amefanya hivyo ili kuokoa muda ambao angeutumia kwenda kufanyiwa kwenye vituo vya masaji vilivyopo mjini.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

No comments:

Post a Comment

 

for more information call us

+255718953088
-------or-------
+255784953088
*email*
innocentfabian@gmail.com
THANKS

quote of the day

"Don't criticize me simply because I am different. Understand me, and you will most likely appreciate my difference and criticize your variance."